Saturday, October 22, 2011
LIVE MATCH SIMBA VS JKT RUVU 2-O
simba imekata mzizi wa fitina baada ya kuchapa jkt ruvu magoli 2kwa bila,magoli ya simba yakitiwa wavuni na felix sunzu na jelly santo
Tuesday, October 11, 2011
Pires wa Cape Verde ashinda Mo Ibrahim

liyekuwa rais wa Cape Verde Pedro Verona Pires ametunukiwa dola za kimarekani milioni tano inayotolewa na wakfu wa Mo Ibrahim kwa ajili ya utawala bora barani Afrika.
Kamati inayoshughulikia zawadi hiyo ilisema Bw Pires, aliyeachia madaraka mwezi Agosti, amesaidia kuifanya nchi hiyo kuwa " yenye demokrasia, utulivu na kustawi zaidi".
Tuzo hiyo intakaiwa kutolewa kila mwaka kwa kiongozi anayechaguliwa kidemokrasia na kuondoka madarakani kwa hiari.
Hapajakuwa na mshindi kwa miaka miwili iliyopita.
Kamati hiyo ilisema hakukuwa na mgombea anayestahili.
Tuzo hiyo ya dola za kimarekani milioni tano, inayotolewa kwa zaidi ya miaka 10, ni zawadi yenye thamani kubwa duniani inayotolewa kwa mtu binafsi.
Washindi wa awali ni aliyekuwa rais wa Botswana Festus Mogae na wa Msumbiji Joaquim Chissano
Monday, October 10, 2011
Kocha awaomba msamaha Waganda
KAMPALA, Uganda
KOCHA wa timu ya Taifa ya Uganda, Bobby Williamson amewaomba msamaha mashabiki wa soka wa Uganda baada ya timu yake kusndwa kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika 2012.
Hakuna mchezaji wa Uganda hata mmoja aliyekuwa na moyo wa kutoka kwenye vyumba vya kubadilishia nguo juzi kwenye uwanja wa Namboole baada ya timu yao kutoka sare ya 0-0 na Kenya na hivyo kushindwa kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika 2012.
Hivi sasa Uganda itabidi isubiri mwaka mmoja mwingine ili iweze kutafuta nafasi ya kufuzu kushiriki Fainali za Afrika zitakazofanyika 2013.Wachezaji wengi wa Uganda walikuwa wakilia na kuhuzunika huku wakishindwa kuamini kilichowatokea ndani ya dakika 90 zac mchezo wakati walitakiwa kushinda ili wafuzu.
Kocha wa Uganda, Bobby Williamson ambaye alitua nchini humo miaka mitatu iliyopita akiwa na kauli ya kuhakikisha Uganda inafuzu fainali za Afrika, pia alishindwa kuamini kilichotokea.
"Nawatakia Angola fainali bora za Afrika,"Bobby Williamson.
"Siwezi kujadili hali yangu ya baadaye hivi sasa, ila nipo Uganda kwa ajili ya soka ya Uganda ambapo naamini nimeweza kuibadilisha,"alisema Bobby Williamson.
"Nawashukuru mashabiki waliojitokeza kwa idadi kubwa na nawaomba msamaha, pia namshukuru raisi na nawashukuru mawaziri na wabunge kwa kujitokeza," alisema Bobby Williamson.
Alisema,"mimi ninapenda kufanya kazi ya soka na ninapenda kufanya kazi na waganda, ninaamini nitaendelea kuwapo mpaka Shirikisho la Soka la Uganda litakaponiambia halinihitaji."
"Mbio zetu za kuwania kufuzu kushiriki fainali za Afrika zilikuwa nzuri, tunao mashabiki wazuri na tunao wachezaji ambao wanafunga magoli, ninawasikitikia vijana wangu ambao walijitahidi sana katika harakati zetu za kuwania kufuzu, lakini juhudi zao zimeshindikana dakika za mwisho,"alisema Bobby Williamson.
Naye kocha wa timu ya Taifa ya Kenya, Zedekiah Otieno alisema,"Waganda wenyewe itabidi wajilaumu, walipata nafasi nyingi, lakini walishindwa kuzitumia."
Wachezaji Brian Umony, Moses Oloya, Mike Sserumaga, Geoffrey Massa wote walipata nafasi za kuifungia Uganda, lakini hawakuzitumia vizuri.
Saa 24 kabla ya mechi hiyo kocha Bobby Williamson alimtimua mshambuliaji hatari wa Uganda, David Obua kwenye timu kwa kile alichodai ukosefu wa nidhamu.
Kabla ya mechi kitendo hicho hakikoonekana na madhara, lakini baada ya mechi mashabiki wa Uaganda walianza kumlaumu Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka la Uganda FUFA kwa kukubali mchezaji huyo kutimuliwa kwenye kikosi.
Kitendo cha kutimuliwa Obua kilichukuliwa na mashabiki kwamba ndiyo sababu kubwa iliyofanya Uganda kushindwa kushinda mechi hiyo.Wakati huo huo timu kubwa zilizoshindwa kufuzu mpaka sasa ni Nigeria, Afrika Kusini, Misri, Cameroon.
Timu ambazo tayari zimeishafuzu ni Zambia, Ghana, Guinea, Angola, Senegal, Mali, Burkina Faso, Niger, Ivory Coast, Botswana, Tunisia wakati Libya ina uhakika wa kupata nafisi ya kufuzu ikiwa timu ambayo imefanya vizuri na kushika nafasi ya pili.
KOCHA wa timu ya Taifa ya Uganda, Bobby Williamson amewaomba msamaha mashabiki wa soka wa Uganda baada ya timu yake kusndwa kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika 2012.
Hakuna mchezaji wa Uganda hata mmoja aliyekuwa na moyo wa kutoka kwenye vyumba vya kubadilishia nguo juzi kwenye uwanja wa Namboole baada ya timu yao kutoka sare ya 0-0 na Kenya na hivyo kushindwa kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika 2012.
Hivi sasa Uganda itabidi isubiri mwaka mmoja mwingine ili iweze kutafuta nafasi ya kufuzu kushiriki Fainali za Afrika zitakazofanyika 2013.Wachezaji wengi wa Uganda walikuwa wakilia na kuhuzunika huku wakishindwa kuamini kilichowatokea ndani ya dakika 90 zac mchezo wakati walitakiwa kushinda ili wafuzu.
Kocha wa Uganda, Bobby Williamson ambaye alitua nchini humo miaka mitatu iliyopita akiwa na kauli ya kuhakikisha Uganda inafuzu fainali za Afrika, pia alishindwa kuamini kilichotokea.
"Nawatakia Angola fainali bora za Afrika,"Bobby Williamson.
"Siwezi kujadili hali yangu ya baadaye hivi sasa, ila nipo Uganda kwa ajili ya soka ya Uganda ambapo naamini nimeweza kuibadilisha,"alisema Bobby Williamson.
"Nawashukuru mashabiki waliojitokeza kwa idadi kubwa na nawaomba msamaha, pia namshukuru raisi na nawashukuru mawaziri na wabunge kwa kujitokeza," alisema Bobby Williamson.
Alisema,"mimi ninapenda kufanya kazi ya soka na ninapenda kufanya kazi na waganda, ninaamini nitaendelea kuwapo mpaka Shirikisho la Soka la Uganda litakaponiambia halinihitaji."
"Mbio zetu za kuwania kufuzu kushiriki fainali za Afrika zilikuwa nzuri, tunao mashabiki wazuri na tunao wachezaji ambao wanafunga magoli, ninawasikitikia vijana wangu ambao walijitahidi sana katika harakati zetu za kuwania kufuzu, lakini juhudi zao zimeshindikana dakika za mwisho,"alisema Bobby Williamson.
Naye kocha wa timu ya Taifa ya Kenya, Zedekiah Otieno alisema,"Waganda wenyewe itabidi wajilaumu, walipata nafasi nyingi, lakini walishindwa kuzitumia."
Wachezaji Brian Umony, Moses Oloya, Mike Sserumaga, Geoffrey Massa wote walipata nafasi za kuifungia Uganda, lakini hawakuzitumia vizuri.
Saa 24 kabla ya mechi hiyo kocha Bobby Williamson alimtimua mshambuliaji hatari wa Uganda, David Obua kwenye timu kwa kile alichodai ukosefu wa nidhamu.
Kabla ya mechi kitendo hicho hakikoonekana na madhara, lakini baada ya mechi mashabiki wa Uaganda walianza kumlaumu Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka la Uganda FUFA kwa kukubali mchezaji huyo kutimuliwa kwenye kikosi.
Kitendo cha kutimuliwa Obua kilichukuliwa na mashabiki kwamba ndiyo sababu kubwa iliyofanya Uganda kushindwa kushinda mechi hiyo.Wakati huo huo timu kubwa zilizoshindwa kufuzu mpaka sasa ni Nigeria, Afrika Kusini, Misri, Cameroon.
Timu ambazo tayari zimeishafuzu ni Zambia, Ghana, Guinea, Angola, Senegal, Mali, Burkina Faso, Niger, Ivory Coast, Botswana, Tunisia wakati Libya ina uhakika wa kupata nafisi ya kufuzu ikiwa timu ambayo imefanya vizuri na kushika nafasi ya pili.
TAIFA STARS HOI,YAPIGWA 3-1 NA MOROCO
Kiumbe mpya kubaini asili yetu



Kiumbe mpya kubaini asili yetu
Mabaki ya kale ya viumbe wawili waliopatikana huko Afrika ya kusini wanaofanana na binadamu yanaweza kubadili mtazamo wetu kuhusu asili yetu.
australopithecus sediba
Babu australopithecus sediba
Mabaki hayo yanayokadiriwa kuwa yamepatikana baada ya miaka milioni 1.9 yalielezewa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 2010, na kupewa jina la kitaalamu Australopithecus sediba.
Tangu hapo kundi la wataalamu lililofanya ugunduzi wakati ule limerudi na uchambuzi wa kina zaidi.
Kundi hilo limelifahamisha jarida linalochapisha habari za Sayansi kua maumbile yaliyoshuhudiwa ya ubongo, miguu, mikono na mifupa ya nyongo yote yameonyesha kama viumbe hawa ni wa kwanza katika asili yetu -binadamu - ama kwa jina la kitaalamu - Homo sapiens.
Profesa Lee Berger wa Chuo kikuu cha Witwatersrand mjini Johannesburg anasema kuwa "wamechunguza sehemu muhimu za binadamu zinazoelezea umbo linalombainisha binadamu na viumbe wengine, na kuna uwezekano wa sehemu za binadamu kukuwa kwa nyakati tofauti na A.sediba anaonyesha kutimiza vigezo vya maumbile ya mwanadamu, kiongozi wa kundi la wataalamu aliifahamisha BBC.
Ni madai makubwa, na ikiwa yana ukweli, basi kuna uwezekano wa rekodi zilizokuepo kuhusu asili yetu kuwekwa kando.
Nadharia inashikilia msimamo kuwa binadamu wa sasa anaweza kudai urithi wake kutoka kwa kiumbe anayejulikana kama Homo erectus aliyeishi zaidi ya miaka milioni moja iliyopita.
homo erectus
kiumbe aliyekwenda kwa miguu miwili
Mnyama huyu, kwa mujibu wa wataalamu wa anthropolojia, huenda naye alikua na asili ya aina ya kiumbe ambaye hakustaarabika ajulikanaye kama hominin, mfano ni Homo habilis au Homo rudolfensis.
Jambo la kuridhisha kuhusu madai juu ya A. sediba ni kwamba ingawa ni wa kale kuliko wenzake , baadhi ya maumbile yake na uwezo wake yanaonyesha kuwa alikuwa na uwezo zaidi kuliko wenzake wa baadaye.
Kwa kifupi inaaminika A.sediba yuko karibu zaidi na babu wa mwanadamu Homo erectus.
babu wa miguu miwili
homo erectus
Mabaki ya sediba yalifukuliwa huko Malapa katika eneo maarufu la asili ya mwanadamu , nje kidogo na kaskazini magharibi mwa Johanesburg.
Viumbe hawa waliotambuliwa kama mwanamke my mzima na mvulana kijana, wametambuliwa kuwa mama na mwana. Kilichobainika ni kuwa walifariki kwa pamoja kufuatia ajali iliyowasababisha kudondoka ndani ya mfumo huo wa shimo kuu au walikwama humo ndani.
Baada ya kufariki, miili yao ilisukumwa ndani ya shimo lenye tope na kuganda humo kwa mda mrefu kama mabaki ya wanyama wengine yaliyokwama humo.
Sunday, October 9, 2011
Makala ya biashara

Mfanyabiashara wa Ghana Herman Kojo Chinery-Hesse, hujulikana kama Bill Gates wa Ghana,na ni wa kwanza kutajwa katika mfululizo maalum wa vipindi vya BBC "African Dream" yaani ndoto ya Afrika ambavyo vinaangaza wajasiriamali wa bara la Afrika.
Kampuni ambayo Bw Chinery-Hesse aliibuni kwa ushirika miongo miwili iliyopita , SOFTtribe Limited, huenda ikawa haijajitanua duniani kama ile kampuni ya Microsoft lakini imeimarika na kuwa mojawapo wa mashirika makubwa ya programu za kompyuta katika Afrika ya Magharibi.
"siku zote nilitaka kuwa mjasiriamali . Nikidhani ndio njia muwafaka ya kuiendeleza Afrika na kujitajirisha ," ameiambia BBC.
Bw Chinery-Hesse alisamehe fursa ya kujiendeleza kimaisha nchini Marekani alikosoma au Uingereza ambako aliwahi kufanya kazi kwa miaka michache ,na badala yake kuamua kuanzisha biashara nchini Ghana.
Alianza kuandika programu za kompyuta chumbani alikolala katika nyumba ya wazazi wake katika wakati ambapo sio watu wengi walitambua umuhimu wa mapinduzi ya kompyuta barani Afrika.
"ilikua ni vigumu sana. Sikutaka kurejea ng'ambo kwa sababu kugeuzwa kuwa raia wa daraja la pili si kitu ambacho kilinivutia," alisema.
Kampuni yake hatimae ikaanza kuunda programu za kompyuta za uongozi wa biashara na sasa ina zaidi ya wateja 250,mkiwemo mashirika kadhaa ya kimataifa kama vile Ford Foundation, Nestle, na Unilever.
SOFTtribe Limited pia ni mshirika wa maendeleo wa kampuni ya Microsoft katika kanda.
"imekua kama burudani. Si rahisi lakini si kusema haiwezekani. Sidhani kuwa mimi ni mtu mwenye kipaji. Nadhani mtu yeyote anaweza kufanya hayo awe makini na awe tayari kusubiri miaka. Mbinu niliyotumia ni kwamba nilijihusisha katika biashara nikiwa sitarajii kuwa tajiri katika kipindi cha miaka 2 ," Bw Chinery-Hesse aliiambia BBC.
"wakati fulani kwa kipindi cha miezi sita kampuni yetu haikupokea hundi zozote na ilitulazimu kugawana kiasi kidogo cha pesa tuliokua nazo. Kulikua na nyakati ambapo hatukua na fedha zozote kulipa mishahara wakati tulipokua na madeni."
Kwa maoni yake miongoni mwa vitu viwili muhimu katika biashara ni ustahamilivu na uaminifu .
"Katika biashara yoyote;lazima uamini kwamba inanufaisha kote kote. Mtu anaenunua lazima anufaike na wewe pia lazima unufaike,la sivyo haitaendelea ."
Hapana shaka Mojawapo wa sababu za kufanikiwa kampuni yake ni kwamba kuanzia mapema sana aliamua kubuni programu ya kompyuta ambayo imetengenezwa mahsusi kwa mazingira ya bara la Afrika.
"nadhani kuna fursa kubwa sana barani Afrika,hali ya umasikini mkubwa,kuna mengi ambayo hayakufanywa ;lakini hii si sayansi ngumu,ukiwa na nidhamu,usiogope kujitosa. ," Bw Chinery-Hesse anawaambia wengine wanaozingatia kua wajasiriamali.
"inawezekana , na nadhani ingewapasa watu wengine kufanya hivyo, na kama hatutajichukulia hatua ,basi wageni watakuja Afrika kama tunavyoona na watafanya wakitakacho"
African Dream hutangazwa na kipindi cha BBC Network Africa kila Jumaatatu. .
Kila wiki mfanyabiashara aliyefanikiwa ataeleza jinsi alivyoanza na funzo gani wengine wanaweza kulipata kutoka kwake.
source
bbc
JUMA PONDAMALI MENSAH: Kipa aliyefungiwa mara tano na mara nne mapambano yalivunjika

Aliyekuwa kipa wa zamani Juma Pondamali
JUMA PONDAMALI MENSAH: Kipa aliyefungiwa mara tano na
mara nne mapambano yalivunjika
KENNEDY MWAISABULA
WAPO makipa kama Peter Manyika, Chachala Muya, Kichochi Kilembe, Abdul Kipenga, Spear Mbwembwe, Issa Manofu na wengineo walitaka kumuiga Juma Pondamali Mensah kwa vituko na mbwembwe zake akiwa langoni, lakini hawakufikia hata robo yake.
Pondamali alikuwa ni wa aina ya kipekee ndani ya nchi hii , ambaye kwa sasa ndio anaowanoa makipa takribani wote wa Taifa Stars akimsaidia Mdenmarki, Jan Poulsen.
Pondamali ambaye alizaliwa mwaka 1957 jijini Dar es Salaam katika Hospitali ya Ocean Road, elimu yake ya msingi aliipata Mlimani na baadaye Karume kabla ya elimu yake ya Sekondari kuipata Mzizima na muda wote huo wa utoto wake soka likiwa ndani ya damu yake.
STANCULESCU VICTORIA AITA WENYE VIPAJI JANGWANI
Kocha raia wa Romania, Victor Stanculescu mwanzoni mwa miaka ya 70 baada ya kuona wachezaji wa Yanga umri wao unasogea aliita watoto wote wenye vipaji wenye umri wa Kids yaani miaka 14 na 15 ili waje wachukue nafasi za wakongwe na ndipo walipojitokeza watoto takribani mia na kupatikana wachache akina Mohamed Mkweche, Adolf Richard, Kasimu Manara, Mohammed Tostao, Gordian Mapango na Juma Pondamali na wengineo ambao kwa maelezo ya Victor aliwatabiria kuwa wote lazima watacheza timu ya Taifa na ndicho hatimaye kilitokea. Pondamali na wenzake walipandishwa hadi kikosi cha pili na baadaye mwaka 1974 walipandishwa hadi kikosi cha kwanza na Pondamali akiwa kipa wa tatu akifuatiwa na wakongwe Muhidini Fadhili na Elias Michaek na kutengeneza muziki mzito ndani ya vijana wa Jangwani na walifanya vizuri mwaka 1974 kwa kuwafunga mahasimu wao na mwaka uliofuatia kuchukua ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati na balaa lilitokea katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika na kutolewa na Enugu Rangers ya Nigeria.
NINI CHANZO CHA MGOGORO ULIOUWA YANGA NA KUUNDA PAN
Matatizo ya wanachama kufuata mkumbo na kutokupima mambo wakamsikiliza kocha wa Zaiere, Tambwe Leya na kuwapuuza wachezaji kwa kila jambo ambalo Tambwe aliwaambia,baada ya ile mechi ya kwanza kule Nigeria kutoka sare kocha aliapa kuwa ni lazima wataiondosha katika mashindano Enugu na baada ya kutolewa akashusha lawama nzito kwa wachezaji akina Boi Iddy, Sunday Manara, Omary Kapera, Gibson Sembuli kuwa wameihujumu timu kwa hiyo na kwamba wanachama waamue moja atoke yeye au wachezaji ndipo wachezaji walipotimka kwa kuzingatia kuwa hatukuona kosa lao.
Wakubwa wote wakaenda kuunda timu inayoitwa Nyota Afrika ya Morogoro na wale waliokuwa watoto wakajiunga na Pilsner ya Dar es Salaam na baada ya mwaka akina Sembuli wakarudi kuungana na vijana wao ambao ndio walikuwa sasa moto wa kuotea mbali na kuunda Pan African kwa mashart kuwa wale vijana wote wapewe kazi na kweli wote waliajiriwa kiwanda cha Madawa, hivyo ndivyo ilivyoundwa Pan ikiwa chini ya mzee Tabu Mangara na Shiraz Sherrif.
MATATIZO ALIYOKUMBANA NAYO SAID EL MAAMRY VITUKO NA UKOROFI WA PONDAMALI
Kama kuna watu waliokuwa wakorofi ndani ya uwanja na wapole kabisa tena waungwana nje ya uwanja basi ni Juma Pondamali. Hawa akina Haruna Moshi, Athuman Idd au Juma Kaseja wanasingiziwa tu, lakini kamwe Pondamali hakuachwa timu ya Taifa.
Mwenyekiti wa FAT wakati huo alishamfungia Pondamali mara tano kwa utovu wa nidhamu ikiwa ni hasa kupiga waamuzi ambao walikuwa wanaacha majukumu yao na kutoa maamuzi ambayo yeye kwake aliona si sahihi.
Mechi alizofungiwa ni ile ya Mwanza kati ya Pan na Tumbaku alifungiwa miezi mitatu, Pan na Simba alifungiwa miezi sita pia alifungiwa miaka mitano kwa kuanzisha fujo nzito kati ya Pan na Simba tena mechi zote hizo zilivunjika mapema tu kutokana na fujo za Pondamali lakini adhabu ile alisamehewa na FAT ya El Maamry baada ya kutangaza kuwa anaachana na soka kabisa, haukupita muda pale mjini Songea tena Pan na Majimaji alileta vurugu kubwa lakini mechi iliendelea na yeye kufungiwa mwezi mmoja. Pondamali tena alifanya balaa jingine kubwa mjini Arusha kati ya Pan na Kiltex tena akiwa mchezaji wa akiba baada ya kuingia uwanjani na kumpiga ngwala refa na pambano kuvunjika.
Vituko vya Pondamali vilikuwa ni hatari kuviona bora usimuliwe aliwahi kupewa kadi ya njano baada ya kudaka shuti kali la Mustafa Nagari wa Sudan na kulibana katikati ya miguu na kushika kichwa na mwamuzi alidhani ni bao na baadaye akawaonyesha mashabiki mpira,hizo ni mbwembwe za Pondamali ambazo hakuiga kwa mtu ingawa anasema na Mambosasa naye alikuwa na vitu kama hivyo ingawa si vingi
ANAMSHUKURU SUNDAY KAYUNI
Baada ya kucheza Yanga 1986 hadi 1991 na mwaka 1992 kupandisha Pan tena na kuambiwa mzee alitimkia AFC Leopards ya Kenya alikoitwa na rafiki yake kipenzi Mahamud Abass aliyekuwa Kenya One na kufikia kwanza timu ya Luo Union kama njia tu , na kukipiga pale hadi mwaka 1996 alipoamua kuachana na soka na kuelekea Muheza kuwa mkulima, ndipo kocha maarufu hapa nchini ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Sunday Kayuni alipomwita na kumlazimisha kuchukua mafunzo ya ukocha mwaka 1997 pale Tandika Mabatini.
"Namshukuru sana Kayuni," anasisitiza Juma Pondamali maarufu kama Mensah, mwenye familia ya watoto wanane ambao ni Kinyanjui, Salama ambaye yuko Uingereza, Masiku, Nassoro, Babby, Fammy ambaye anafuata nyayo zake katika soka, Mensah na Mussa na mkewe ambaye ni raia wa Uingereza
MECHI ISIYOTOKA KICHWANI KWAKE DAIMA
Pondamali anazungumzia kwa hisia kali kuwa mechi ambayo hatoisahau ni ile waliyocheza na Zambia na kuwapeleka Lagos katika fainali za Mataifa ya Afrika. anasema Wazambia walikuwa ni balaa maana kuna wakati nusu saa nzima mpira ulikuwa katika goli la Stars na yeye ilikuwa ni kuokoa tu na kubutua mbele na wenyewe wanaweka chini wanakuja ilikuwa ni balaa, "Mazambia yale yalikuwa yanaongozwa na Godfrey Chitalu, Obby Kapita, Pele Kaimana, Hakimu Musenge ilikuwa ni shughuli pevu."
Pondamali ambaye ni shabiki wa Barcelona na Real Madrid anakumbuka Taifa Stars iliundwa na yeye, Leopard Tasso, Mohammedy Kajole, Leodegar Tenga, Salim Amir, Jella Mtagwa, Omary Hussen, Thueni Ally, Adolf Rishard, Peter Tino, Mohammed Salum na kocha alikuwa kutoka Poland akisaidiwa na Joel Bendera.
WALIVYOPIGANA MATAIFA HURU LAGOS NIGERIA 1980
�Chini ya kocha Mpoland na msaidizi wake Bendera timu iliweka kambi Mexico na moja kwa moja kuelekea Nigeria kupigana katika kundi la kifo na timu zenye wachezaji wengi wa kulipwa kasoro Tanzania, ikiongezewa nguvu na Ahmed Amasha, Juma Mkambi, Mtemi Ramadhani na Mohamedy Bakari Tall, tukiumana na Misri,wenyeji Nigeria na Ivory Coast jambo ambalo hadi leo mwaka wa 29 vijana wameshindwa kufika huko na wala kutoa wachezaji bora kama ilvyokuwa kwa Omary Mahadhi na Maulid Dilunga,� anasema mkongwe huyo.
JE SOKA LIMEMSAIDIAJE
Ana shamba Muheza, Tanga na alijenga nyumba Mburahati, Dar es Salaam na sasa anaishi Kigamboni ambako watoto wake walimnunulia nyumba na kupitia ukocha ana viwanja viwili Bunju, jijini Dar es Salaam ambako atakuwa anaishi baadaye lakini soka limemfanya kujuana na watu wengi.
Huyo ndiye Pondamali aliyezaliwa Dar, kukulia Dar na sasa anazeekea Dar.
Mwandishi wa makala hii ni mchambuzi wa soka na anafanya kazi Bandari anapatikana 0652875794 au Email kennymwaisabula@yahoo.com
source
mwanaspoti
Boeing kuwasilisha 787 ya kwanza kabisa



Kampuni ya utengenezaji ndege ya Marekani - Boeing - itawasilisha rasmi ndege ya kwanza aina ya 787 Dreamliner kwa shirika la ndege la All Nippon Airways (ANA) la Japan
.Awali Dreamliner ilipangwa kuwa tayari mwaka 2008, lakini Boeing imekumbwa na mflulizo wa vikwazo, ambapo hivi karibuni moto uliwaka ndani ya ndege za majaribio mwezi Januari.
Ndege hiyo isiyotumia mafuta mengi imetengenezwa kwa kutumia malighafi nyepesi.
Boeing inapanga kutengeneza ndege 10 kwa mwezi kuanzia mwaka 2013.
Ndege hiyo itakabidhiwa kwa ANA katika kitongoji cha Everett, Washington kabla ya kuruka na kwenda Tokyo ambapo itawasili siku ya Jumatano.
Dreamliner
Dreamliner
Boeing imesema ndege hiyo yenye safu mbili na ukubwa wa kati ina madirisha makubwa na hali nzuri ya unyevunyevu ndani ya ndege na hewa safi hali ambayo itaruhusu abiria kuwasili wanapokwenda wakiwa katika njema zaidi.
Lakini matatizo ya Dreamliner yameharibu sifa ya Boeing, na kampuni hiyo ina matumaini kuwa uzinduzi wenye mafanikio utasaidia kufuta ucheleweshwaji uliotokea.
Mashaka
Makamu wa rais wa masuala ya masoko wa Boeing, Randy Tinseth ameiambia BBC: "Huu ni mradi ambao umetoka mbali. Tunaamini itakuwa ndege nzuri.
"Hatimaye tunaona matumaini ya maelfu ya 787 katika siku za mbele."
Alipoulizwa sababu za kuchelewa kutoka kwa ndege ya Boeing 787 Bw Tinseth amesema "kuna mashaka katika kila ndege mpya".
Amesema: "Tumetumia fedha zaidi katika ndege hii kuliko tuliyotarajia, lakini kwa mara nyingine tena bado tupo katika nafasi nzuri, tunaamini mradi huu utaendelea kuwa na faida."
Uzalishaji
Uzalishaji wa Dreamliner kwa sasa unatoa takriban ndege 2.5 kwa mwezi.
Mpaka sasa ndege zipatazo 821 aina ya 787 zinatakiwa kununuliwa kutoka Boeing, ambayo inasema inatumia 20% pungufu ya mafuta yanayotumiwa na ndege za kawaida za ukubwa huo.
Dreamliner
Boeing na Airbus
Ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 290 katika ndege yake kubwa ya 787-9, lakini 787 ni ndogo kuliko jumbo jet 747 ya Boeing.
Hata hivyo, Boeing inadhani kuwa 787 itakuwa maarufu katika makampuni ya ndege, kwa kuwa itakuwa na uwezo wa kuruka moja kwa moja kwenda katika viwanja vidogo vya ndege.
Mahasimu
Mahasimu wa Boeing wa Ulaya, Airbus, kwa sasa inatengeneza mshindani wa moja kwa moja wa 787, iitwayo Airbus A350 XWB.
Airbus imepokea maombi ya ununuzi yanayozidi ndege 550 ya A350 XWB, lakini ndege hiyo haitakuwa tayari hadi mwaka 2013.
ANA inatazamia kuanza kutumia ndege ya kwanza aina ya 787 katika safari kutoka Tokyo kwenda Okayama-Hiroshima tarehe 11 Novemba.
Baadaye itaruisha ndege hiyo kimataifa kutoka Tokyo kwenda Frankfurt Ujerumani, mwezi Januari.
"Watu wengi wanasema kuwa ndege hii [787] itakuwa maarufu sana," amesema George Hamlin, rais wa taasisi ya washauri wa usafirishaji ya Hamlin.
Heh! Ray C atakubali kweli?

'
MAMA mzazi wa mwanamuziki Rehema Chalamila 'Ray C' amesema ana imani kubwa kwamba ipo siku mwanaye huyo atafuata nyayo zake kwa kuokoka na kuachana na mambo ya dunia.
"Mimi nimeokoka na watoto wangu pia wameokoka, lakini amebaki Ray C ambaye hata hivyo kila siku nimekuwa nikimuomba Mungu naye amjalie aokoke ili aweze kumtumikia Mungu kikamilifu," Mama Chalamila alimwambia rafiki yake Ray C mjini Iringa wikiendi iliyopita na Mwanaspoti kuinasa kauli hiyo ingawa mama huyo hakupenda kuingia kiundani.
Habari zinasema kuwa mama huyo amekuwa akikabiliana na wakati mgumu licha ya nia yake ya kutaka kumbadili mwanaye ambaye ni mwanamuziki nguli wa kidunia.
Msanii huyo imeelezwa kuwa kwa sasa yupo nchini Marekani kikazi na makazi yake amehamishia jijini Nairobi, Kenya.
Diamond alimkusudia kabisa Wema

MSANII wa muziki wa Bongo, Diamond, amesema kitendo cha kumvisha pete ya uchumba mlimbwende na muigizaji wa filamu za Bongo, Wema Sepetu, hajakifanya kwa makisio bali amekusudia na ameona anafaa kuwa mke wake.
Uamuzi huo aliuweka wazi katika siku yake ya kuzaliwa iliyofanyika katika Ukumbi wa Maisha Club jijini Dar es Salaam, akisema kuwa Wema ni mwanamke aliye na umuhimu mkubwa katika maisha yake.
"Nimekuwa na uhusiano na wadada wengine lakini huyu Wema nawahakikishia kuwa ni muhimu sana kwangu na pia anastahili kuwa mke wangu na ndiyo maana leo nimeamua kuweka hadharani mwanzo wa uhusiano huu," alisema Diamond.
Diamond anayetamba na wimbo wa Moyo Wangu pamoja na vibao vingine kama Mbagala na Kamwambie, akionekana mwenye furaha na akasisitiza kuwa ataharakisha kufunga ndoa na Wema.
Wakenya wanamuaga Wangari Maathai

Maiti ya Wangari Maathai imechomwa moto mjini Nairobi, kama alivyousia.
Kabla ya hapo Bibi Maathai, aliyefarika mwezi uliopita kutokana na saratani, aliagwa kwa maziko ya kitaifa.
Bibi Maathai aliwahi kupata tuzo ya amani ya Nobel, na alikuwa maarufu kwa kazi yake ya kutetea wanawake na mazingira.
Ibada ya wafu ilifanywa kwenye bustani ya Uhuru Park, Nairobi, ambayo Wangari aliitetea sana wakati serikali ya Rais Moi ilipotaka kuruhusu majumba kujengwa katika bustani hiyo.
Maelfu ya watu walifurika katika bustani hiyo, wakiongozwa na kiongozi wa Kenya, Rais Mwai Kibaki.
Wanaharakati wa mazingira na wanawake ambao walishirikiana na Bibi Maathai tangu alipoanza kampeni zake miaka ya 1970 piya walihudhuria, pamoja na wawakilishi kutoka nchi za nje.
Tanzania iliwakilishwa na Waziri wa Makaazi, Bibi Anna Tibaijuka, ambaye piya alikuwa rafiki wa Bibi Maathai; Sudan ilituma mwakilishi, na wanabalozi wa nchi kadha walihudhuria.
Baadhi ya waombolezi walibeba miche ya miti ili kuipandisha hapo bustanini; na familia yake iliotesha mti wa kiasili ili kubakisha kumbu-kumbu ya marehemu.
Kukumbuka msimamo wake wa kutotaka miti kukatwa, jeneza lake limetengenezwa kwa magugu ya majini, kili, na mwanzi
Katika miaka ya 1970 Bibi Wangari Maathai alianzisha shirika la Greenbelt Movement, ambalo lengo lake lilikuwa kuwapunguzia shida akina mama, ili waweze kupata kuni na maji safi kwa urahisi.
Tangu wakati huo karibu miti milioni 50 imepandishwa Kenya.
Maelfu itapandishwa siku zijazo kama kumbukumbu kwa mawanamke aliyegusa nyoyo za watu wa Kenya na dunia nzima.
Bibi Maathai piya alipigania wafungwa wa kisiasa waachiliwe.
source bbc
Uhuru: Hakuna kama Cannavaro Bongo
MSHAMBULIAJI wa Simba, Uhuru Suleiman, amefunguka na kuweka wazi kilicho moyoni mwake kwa kusema Nadir Haroub �Cannavaro� wa Yanga ndiye mfalme wa nafasi ya beki ya kati kwa Tanzania na hana mpinzani.
Uhuru ametamka hilo kwa maelezo kuwa amefanya utafiti wake kama mshambuliaji kwa miezi 13 akiwaangalia mabeki tofauti katika michuano mbalimbali iliyopita.
Akizungumza na na mwandishi wetu, Uhuru alisema; "Tanzania kuna mabeki wengi, lakini kwa sasa hakuna kama Cannavaro, na kwamba huyo ni zaidi ya wote utake, usitake."
"Mimi ni mshambuliaji, najua beki gani wa kuogopwa, kumpita Cannavaro lazima ufanye kazi kubwa na ndiyo maana nasema, Tanzania kwa sasa hana mpinzani, wengine watafuata, naamini ninachokizungumza na hii ni baada ya utafiti wangu wa miezi 13 sasa."
Cannavaro, ambaye pia huchezea Zanzibar Heroes, aliitwa dakika za mwisho kwenye kikosi cha Taifa Stars na kufanya mazoezi ya siku moja kabla ya kuondoka na kuelekea Morocco kwa mechi ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika baada ya Victor Costa kuumia nyonga.
Akizungumzia hilo, Uhuru alisema kuwa;" Haijalishi, lakini ieleweke kuwa anastahili kuwepo na kama asingekuwepo, kungekuwa na pengo kubwa.
Uhuru ametamka hilo kwa maelezo kuwa amefanya utafiti wake kama mshambuliaji kwa miezi 13 akiwaangalia mabeki tofauti katika michuano mbalimbali iliyopita.
Akizungumza na na mwandishi wetu, Uhuru alisema; "Tanzania kuna mabeki wengi, lakini kwa sasa hakuna kama Cannavaro, na kwamba huyo ni zaidi ya wote utake, usitake."
"Mimi ni mshambuliaji, najua beki gani wa kuogopwa, kumpita Cannavaro lazima ufanye kazi kubwa na ndiyo maana nasema, Tanzania kwa sasa hana mpinzani, wengine watafuata, naamini ninachokizungumza na hii ni baada ya utafiti wangu wa miezi 13 sasa."
Cannavaro, ambaye pia huchezea Zanzibar Heroes, aliitwa dakika za mwisho kwenye kikosi cha Taifa Stars na kufanya mazoezi ya siku moja kabla ya kuondoka na kuelekea Morocco kwa mechi ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika baada ya Victor Costa kuumia nyonga.
Akizungumzia hilo, Uhuru alisema kuwa;" Haijalishi, lakini ieleweke kuwa anastahili kuwepo na kama asingekuwepo, kungekuwa na pengo kubwa.
Tuesday, October 4, 2011
4 oct Siwahitaji:Ferdinand, Defoe walia na Capello
Mmoja ya wachezaji ambao hawaitajiki na Capello, Rio Ferdinand
LONDON, ENGLAND
JERMAIN Defoe na Rio Ferdinand hawamo katika kikosi cha kocha wa England, Fabio Capello kitakachocheza mechi ya kufuzu fainali za Mataifa ya Ulaya dhidi ya Montenegro, Ijumaa wiki hii.
Miezi sita iliyopita Ferdinand alikuwa nahodha wa England na Defoe ambaye ameanza kasi kwa kufunga mabao matatu katika mechi nne zilizopita, ameshangaa kwa nini hajaitwa. Mchezaji huyo wa Tottenham alisema: "Nimekosa amani baada ya kutemwa." �Naamini sijawahi kumwangusha Capello wakati nilipocheza, lakini nitafanya kila niwezalo kuhakikisha ninapata nafasi kwa mara nyingine."
Ferdinand, ambaye ameitwa katika timu ya taifa mara 81 tangu alipoitwa kwa mara ya kwanza chini ya kocha Glenn Hoddle, Novemba 1997, alikuwa nahodha mpaka alipopoteza nafasi mbele ya John Terry, Machi mwaka huu.
Iliaminika kuwa angeitwa katika kikosi baada ya kupona matatizo ya misuli.
Lakini pia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 aliingia kipindi cha pili katika mechi dhidi ya Norwich, ambayo ilitazamwa na Capello.
Capello aliamua kumwacha nyota wa Liverpool, Steven Gerrard baada ya kutokea mvutano na kocha Kenny Dalglish, ambaye anaona kwamba Gerrard hastahili kuingia katika timu ya taifa kwani ndio kwanza amepona maumivu yaliyokuwa yakimsumbua.
Ijumaa iliyopita, Gerrard alikiri kuwa hakutaka kuingia katika timu ya taifa kwa kuwa anaona hajapata mazoezi ya kutosha.
Capello alimuita mshambuliaji wa Manchester United, Danny Welbeck na kipa wa zamani wa West Brom, Scott Carson. Pia alimtaja Bobby Zamora kwa mara ya kwanza tangu alipokosekana katika timu ya taifa mwaka jana kufuatia
LONDON, ENGLAND
JERMAIN Defoe na Rio Ferdinand hawamo katika kikosi cha kocha wa England, Fabio Capello kitakachocheza mechi ya kufuzu fainali za Mataifa ya Ulaya dhidi ya Montenegro, Ijumaa wiki hii.
Miezi sita iliyopita Ferdinand alikuwa nahodha wa England na Defoe ambaye ameanza kasi kwa kufunga mabao matatu katika mechi nne zilizopita, ameshangaa kwa nini hajaitwa. Mchezaji huyo wa Tottenham alisema: "Nimekosa amani baada ya kutemwa." �Naamini sijawahi kumwangusha Capello wakati nilipocheza, lakini nitafanya kila niwezalo kuhakikisha ninapata nafasi kwa mara nyingine."
Ferdinand, ambaye ameitwa katika timu ya taifa mara 81 tangu alipoitwa kwa mara ya kwanza chini ya kocha Glenn Hoddle, Novemba 1997, alikuwa nahodha mpaka alipopoteza nafasi mbele ya John Terry, Machi mwaka huu.
Iliaminika kuwa angeitwa katika kikosi baada ya kupona matatizo ya misuli.
Lakini pia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 aliingia kipindi cha pili katika mechi dhidi ya Norwich, ambayo ilitazamwa na Capello.
Capello aliamua kumwacha nyota wa Liverpool, Steven Gerrard baada ya kutokea mvutano na kocha Kenny Dalglish, ambaye anaona kwamba Gerrard hastahili kuingia katika timu ya taifa kwani ndio kwanza amepona maumivu yaliyokuwa yakimsumbua.
Ijumaa iliyopita, Gerrard alikiri kuwa hakutaka kuingia katika timu ya taifa kwa kuwa anaona hajapata mazoezi ya kutosha.
Capello alimuita mshambuliaji wa Manchester United, Danny Welbeck na kipa wa zamani wa West Brom, Scott Carson. Pia alimtaja Bobby Zamora kwa mara ya kwanza tangu alipokosekana katika timu ya taifa mwaka jana kufuatia
4 oct Kapombe yupo kila mahali Simba
KINDA la Simba, Shomari Kapombe amewapa raha mashabiki wa timu hiyo, baada ya kumwambia kocha wake, Moses Basena amtumie atakavyo ili amfanyie mambo.
Hii ni dalili nzuri kwa simba kuwa imelamba dume baada ya kumsajili nyota huyo kutoka Polisi Morogoro ambaye sasa ni kipenzi cha mashabiki kutokana na kiwango na uimara wa kumudu namba nyingi uwanjani.
Kocha Basena amekuwa akimtumia kwa nafasi tofauti uwanjani kulingana na timu wanayocheza nayo, kiungo na beki, kwa nafasi zote amefanya vizuri na kuwa simulizi mechi inapomalizika.
Aliliambia Mwanaspoti kuwa: ��Mimi sina tatizo, kocha anipange nafasi yoyote, kulingana na chaguo lake, mwenyewe atafurahi. Nina kipaji cha kucheza kwa ufasaha namba zote isipokuwa kipa, namba tatu na 11 naweza japokuwa si sana,��alisema Kapombe aliyeweka wazi namba tano (sentahafu) ndiyo anaipenda zaidi.
Aliongeza kwa kusema, kwa sababu Simba ni timu kubwa ushindani ni mkubwa, lakini atajituma ili apate nafasi ya kumudu kikosi cha kwanza.
source
mwanaspoti
Hii ni dalili nzuri kwa simba kuwa imelamba dume baada ya kumsajili nyota huyo kutoka Polisi Morogoro ambaye sasa ni kipenzi cha mashabiki kutokana na kiwango na uimara wa kumudu namba nyingi uwanjani.
Kocha Basena amekuwa akimtumia kwa nafasi tofauti uwanjani kulingana na timu wanayocheza nayo, kiungo na beki, kwa nafasi zote amefanya vizuri na kuwa simulizi mechi inapomalizika.
Aliliambia Mwanaspoti kuwa: ��Mimi sina tatizo, kocha anipange nafasi yoyote, kulingana na chaguo lake, mwenyewe atafurahi. Nina kipaji cha kucheza kwa ufasaha namba zote isipokuwa kipa, namba tatu na 11 naweza japokuwa si sana,��alisema Kapombe aliyeweka wazi namba tano (sentahafu) ndiyo anaipenda zaidi.
Aliongeza kwa kusema, kwa sababu Simba ni timu kubwa ushindani ni mkubwa, lakini atajituma ili apate nafasi ya kumudu kikosi cha kwanza.
source
mwanaspoti
4Oct NSAJIGWA AUMIA MAZOEZINI STARS
Nahodha wa Taifa Stars, Shadrack Nsajigwa ameumia nyonga (groin) kwenye mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika jana (Oktoba 3 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa daktari wa Taifa Stars, Dk. Mwanandi Mwankemwa, maumivu hayo yatamweka Nsajigwa ambaye pia ni Nahodha wa Yanga nje ya uwanja kwa kati ya wiki mbili hadi nne.
Kutokana na ushauri wa daktari, Kocha Jan Poulsen amemuondoa kwenye kikosi hicho ambacho kitasafiri Oktoba 6 mwaka huu kwenda Casablanca, Morocco kwa ajili ya mechi dhidi ya Morocco itakayochezwa Oktoba 9.
Badala yake Kocha Poulsen amemuita kwenye timu yake Nassoro Masoud Said ‘Cholo’ wa Simba kuziba nafasi ya beki huyo wa pembeni.
Kwa mujibu wa daktari wa Taifa Stars, Dk. Mwanandi Mwankemwa, maumivu hayo yatamweka Nsajigwa ambaye pia ni Nahodha wa Yanga nje ya uwanja kwa kati ya wiki mbili hadi nne.
Kutokana na ushauri wa daktari, Kocha Jan Poulsen amemuondoa kwenye kikosi hicho ambacho kitasafiri Oktoba 6 mwaka huu kwenda Casablanca, Morocco kwa ajili ya mechi dhidi ya Morocco itakayochezwa Oktoba 9.
Badala yake Kocha Poulsen amemuita kwenye timu yake Nassoro Masoud Said ‘Cholo’ wa Simba kuziba nafasi ya beki huyo wa pembeni.
Simba Oparesheni Mauaji
SIMBA iliyotulia kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara kwa pointi zake 18, imeukimbia Uwanja wa Sigara ilipokuwa ikifanya mazoezi na sasa imetua Kinesi, jijini Dar es Salaam lakini uongozi umetangaza rasmi 'Operesheni Mechi Tano.'
Wekundu hao wameondoka Sigara maeneo ya Chang'ombe, Dar es Salaam ambako pia African Lyon wanayokwaana nayo Oktoba 16 inautumia. Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' aliiambia Mwanaspoti jana Jumatatu kuwa; "Tumeanzisha operesheni maalumu tumeipa jina la "Operesheni Mechi Tano' itamhusisha kila Mwanasimba popote kuhakikisha kwamba tunashinda mechi zote tano zilizosalia mzunguko wa kwanza tena kwa kishindo, hiyo ndiyo operesheni ya uhakika baada ya hapo tunatulia tunasubiri mzunguko wa pili kwa raha zetu."
Simba inakabiliwa na mechi tano dhidi ya African Lyon, Ruvu Shooting, JKT Ruvu, Yanga na Moro United.
Simba inaendelea na mazoezi hayo kwa kuwatumia wachezaji 17 isipokuwa Juma Jabu, Juma Kaseja, Juma Nyosso na Victor Costa walioko Taifa Stars, Ulimboka Mwakigwe amefiwa na baba yake mdogo na Haruna Moshi �Boban� anauguliwa na mwanaye.
Kati ya waliofika ni Mnyarwanda, Patrick Mafisango ambaye awali, alisimamishwa na uongozi wa klabu hiyo baadaye akasamehewa na Salum Machaku aliyeondolewa bandeji gumu wiki iliyopita, Gervais Kago wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na Mzambia Felix Mumba Sunzu.
Meneja wa Simba, Abdalah King Kibaden alisema kuwa ; "Tumeanza mazoezi kama kawaida, tumeamua kuhama uwanja kwavile tulikuwa tunabanana na African Lyon, tumeona bora tuhamie Kinesi ni uwanja wetu pia tutapata nafasi zaidi."
Kocha Mkuu Moses Basena aliwasili jana Jumatatu, lakini msaidizi wake, Richard Amatre alisema mazoezini kuwa; "Nimekazania sana mazoezi kwa sababu nataka wachezaji wangu wawe na stamina na hiyo itawasaidia kucheza muda mrefu uwanjani, nguvu za miguu kitu ambacho wengi wao walikuwa hawana.
�Nataka turudi kivingine kwenye ligi baada ya haya mapumziko, na tumepania kucheza mpira wa ufundi zaidi, nguvu na kumuhimili kila mmoja tutakayekutana naye, tutakuwa tunabadilika kila mechi kulingana na timu tutakayokutana nayo ndio maana nataka wachezaji wangu wawe fiti kuliko kawaida,�alisisitiza kocha huyo huku akisema ubora wa viwanja wanavyotumia kuwa ni duni.
Daktari wa timu hiyo Abeid Shindika aliiambia Mwanaspoti kuwa Amir Maftah ameanza mazoezi mepesi na ana asilimia kubwa ya kucheza dhidi ya African Lyon Oktoba 16.
source
© Mwananchi Communications Ltd:2007
Wekundu hao wameondoka Sigara maeneo ya Chang'ombe, Dar es Salaam ambako pia African Lyon wanayokwaana nayo Oktoba 16 inautumia. Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' aliiambia Mwanaspoti jana Jumatatu kuwa; "Tumeanzisha operesheni maalumu tumeipa jina la "Operesheni Mechi Tano' itamhusisha kila Mwanasimba popote kuhakikisha kwamba tunashinda mechi zote tano zilizosalia mzunguko wa kwanza tena kwa kishindo, hiyo ndiyo operesheni ya uhakika baada ya hapo tunatulia tunasubiri mzunguko wa pili kwa raha zetu."
Simba inakabiliwa na mechi tano dhidi ya African Lyon, Ruvu Shooting, JKT Ruvu, Yanga na Moro United.
Simba inaendelea na mazoezi hayo kwa kuwatumia wachezaji 17 isipokuwa Juma Jabu, Juma Kaseja, Juma Nyosso na Victor Costa walioko Taifa Stars, Ulimboka Mwakigwe amefiwa na baba yake mdogo na Haruna Moshi �Boban� anauguliwa na mwanaye.
Kati ya waliofika ni Mnyarwanda, Patrick Mafisango ambaye awali, alisimamishwa na uongozi wa klabu hiyo baadaye akasamehewa na Salum Machaku aliyeondolewa bandeji gumu wiki iliyopita, Gervais Kago wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na Mzambia Felix Mumba Sunzu.
Meneja wa Simba, Abdalah King Kibaden alisema kuwa ; "Tumeanza mazoezi kama kawaida, tumeamua kuhama uwanja kwavile tulikuwa tunabanana na African Lyon, tumeona bora tuhamie Kinesi ni uwanja wetu pia tutapata nafasi zaidi."
Kocha Mkuu Moses Basena aliwasili jana Jumatatu, lakini msaidizi wake, Richard Amatre alisema mazoezini kuwa; "Nimekazania sana mazoezi kwa sababu nataka wachezaji wangu wawe na stamina na hiyo itawasaidia kucheza muda mrefu uwanjani, nguvu za miguu kitu ambacho wengi wao walikuwa hawana.
�Nataka turudi kivingine kwenye ligi baada ya haya mapumziko, na tumepania kucheza mpira wa ufundi zaidi, nguvu na kumuhimili kila mmoja tutakayekutana naye, tutakuwa tunabadilika kila mechi kulingana na timu tutakayokutana nayo ndio maana nataka wachezaji wangu wawe fiti kuliko kawaida,�alisisitiza kocha huyo huku akisema ubora wa viwanja wanavyotumia kuwa ni duni.
Daktari wa timu hiyo Abeid Shindika aliiambia Mwanaspoti kuwa Amir Maftah ameanza mazoezi mepesi na ana asilimia kubwa ya kucheza dhidi ya African Lyon Oktoba 16.
source
© Mwananchi Communications Ltd:2007
4 Oct KALI YA LEO: MASHABIKI WA BAYERN WAKUTWA WAKIFANYA MAPENZI JUKWAANI
Katika hali ya kushangaza mashabiki wa klabu ya Bayern Munich walikutwa wakifanya mapenzi kwenye jukwaa katika mechi ya Bundesliga dhidi Hoffenheim iliyofanyika katika uwanja Neckar-Arena juzi Jumamosi.
Ndani ya dakika 16 tangu mchezo uanze, wapenzi hao waliokuwa katika jukwaa la mashabiki wa Bayern walionekana wakifanya mapenzi.
Wapenzi hao walionekana wakiwa wameshusha nguo za chini huku wakifanya majambozi huku watu wengine waliowazunguka wakionekana kutokushitushwa na tukio lile, lakini haikuchukua muda kabla ya walinzi wa uwanja kuingilia kati na kufanikiwa kuwastopisha na kuendelea na mambo yao.
Wapenzi waliacha kufanya mambo yao baada ya walinzi kuingilia kati lakini katika kipindi cha mapumziko bibi na bwana hao walirudia tena kufanya mapenzi hali iliyopelekea kutolewa amri ya kuwatoa nje ya uwanja na kukamatwa na polisi kwa kosa kufanya mapenzi hadharani.
Ndani ya dakika 16 tangu mchezo uanze, wapenzi hao waliokuwa katika jukwaa la mashabiki wa Bayern walionekana wakifanya mapenzi.
Wapenzi hao walionekana wakiwa wameshusha nguo za chini huku wakifanya majambozi huku watu wengine waliowazunguka wakionekana kutokushitushwa na tukio lile, lakini haikuchukua muda kabla ya walinzi wa uwanja kuingilia kati na kufanikiwa kuwastopisha na kuendelea na mambo yao.
Wapenzi waliacha kufanya mambo yao baada ya walinzi kuingilia kati lakini katika kipindi cha mapumziko bibi na bwana hao walirudia tena kufanya mapenzi hali iliyopelekea kutolewa amri ya kuwatoa nje ya uwanja na kukamatwa na polisi kwa kosa kufanya mapenzi hadharani.
Subscribe to:
Posts (Atom)