tuwasiliane

Monday, December 26, 2016

George Michael aaga dunia

Uingereza
Mwanamuziki nguli mwenye asili ya Uingereza, ambaye alijizolea umaarufu mnamo mwaka 1980 na kuwika ulimwenguni kutokana na mtindo wake wa mahadhi ya pop, amefariki dunia.
George Michael amekufa akiwa na umri wa miaka hamsini na tatu.Msemaji wa mwanamuziki huyo amearifu kwamba nguli huyo aliaga dunia akiwa nyumbani kwake Oxfordshire.
Kundi la Wham lilijipatia umaarufu ulimwengu mzima na kupata mafanikio makubwa kwa tungo zao kama 'Wake Me Up Before You Go-Go' na 'Careless Whisper'
kundi hilo lilijizolea umaarufu na kuwa kundi la kwanza la Magharibi kwa miondoko ya pop kufanya onesho la kimuziki nchini China.
Bendi hiyo iliposambaratika, George Michael aliendelea kujizoelea umaarufu akiwa mwanamuziki wa kujitegemea.
Katika kipindi cha muongo uliopita alikuwa akisumbuliwa na maradhi yasababishwayo na utumizi wa dawa za kulevya, ikiwemo kuendesha gari kwa kasi na kupoteza mwelekeo na kuingia kwenye duka mjini London huku akiwa amelewa dawa za kulevya.

No comments:

Post a Comment