tuwasiliane

Monday, December 26, 2016

KRC GENK YAMTIMUA KOCHA ALIYEMSAJILI SAMATA

screen-shot-2016-12-26-at-12-59-00-pm
Boxing day yako imekujaje leo? basi kwa kocha Peter Maes imekua mbaya kwasababu kibarua chake kimeota nyasi kwenye club ya KRC Genk leo.
Habari kutoka kwenye tovuti maalum ya club ya KRC Genk imetoa taarifa kuhusu kumaliza ushirikiano na kocha huyu baada ya kuanza kuifundisha club hii tangu msimu wa 2015/2016.
Kocha huyu alianza majukumu ya kuifundisha club ya Genk mwaka 2015 hivyo basi ndiye kocha wa kwanza kumpokea Mbwana Samatta kwenye soka la Ulaya.
Genk wamemtakia maisha mema kwenye majukumu yake mengine na maisha baada ya Genk.

No comments:

Post a Comment