Kama nilivyosema, tuna muda mfupi sana kwa ajili ya kufanya usajili, tunafanyia kazi orodha ya wachezaji waliopendekezwa kwa kumalizana nao, ndani na nje ya nchi. Baada ya Joram (Mgeveke), sasa ni Chabalala,”alisema Poppe.
Poppe amewahakikishia wana Simba SC kwamba safari hii watasajili wachezaji bora ambao watarejesha heshima ya klabu hiyo msimu ujao. Jana Simba SC ilikamilisha usajili wa beki wa kati, Joram Mgeveke wa Lipuli ya Iringa ambaye yupo katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars.
Beki huyo alicheza kwa dakika 75 mechi ya kirafiki ya Tanzania na Malawi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambayo bao pekee la Amri Kiemba wa Simba SC liliipa Taifa Stars ushindi wa 1-0 kabla ya kumpisha Kevin Yondan wa Yanga. Tangu hapo, kinda huyo wa miaka 22 amekuwemo kwenye orodha ya wachezaji 18 walioshiriki mechi zote za Stars dhidi ya Zimbabwe kufuzu Mataifa ya Afrika kama mchezaji wa akiba.
No comments:
Post a Comment