tuwasiliane

Saturday, December 24, 2011

24 DEC.AT Sio Mzanzibari...!!


Msanii AT, amesema ameshtushwa sana na kauli ya baaraza la sanaa la kisiwani huko, kwamba yeye sio raia wa Tanzania visiwani na kuanzia sasa kwa sababu msanii huyu kwa sasa anaishi Tanzania Bara, itabidi awe analipia anapokwenda kufanya shoo zake Zanzibar.

AT amesema yeye ni mzaliwa wa Zanzibar, amezaliwa Mwembeladu Unguja na watu wote wanamfahamu akisisitiza kuwa amedhalilishwa sana kwa kuvuliwa uraia na watu wasio na mamlaka ya Uhamiaji.

Msanii huyu alikumbana na maswahiba ya kushushwa jukwaani hivi karibuni huko Unguja alipokuwa akifanya onyesho, na imefahamika kuwa, hata video ya msanii huyu inayojulikana kama ya bao la kete, imefungiwa kuchezwa katika vituo vya televisheni visiwani humo kutokana sababu ziliyoelezwa kuwa ni za kimaadili.

No comments:

Post a Comment