
"Mweusi" mkali wa Hip-Hop Tanzania Joh Makini ameguswa na mafuriko yanayoendelea kuikumba Dar-es-Salaam na wakazi wake na kutoa sifa kwa kituo cha Televisheni cha EATV kwa kuwa karibu na wananchi kwa kuwapatia taarifa za umakini kwa kila kinachoendelea kuhusiana na mafuriko hayo.
Kufuatia EATV kuonesha muhanga mmojawapo wa mafuriko mama wa makamo fundi cherehani aliyepoteza mali zake ikiwemo cherehani, EATV imeandika kupitia ukurasa wake wa twitter kuwa Joh Makini amesema atamnunulia mama huyo cherehani mpya.
No comments:
Post a Comment