tuwasiliane

Sunday, September 3, 2017

“Magoli mawili niliyowafunga Botswana yatanisaidia Morocco” – Msuva

Simon Msuva amesema magoli mawili aliyofunga kwenye mechi dhidi ya Botswana yatamsaidia kujiamini katika klabu yake ya Difaa El Jadid pindi atakaporejea Morocco.
Msuva amecheza katika kiwango cha juu dhidi ya Botswana na kufanikiwa kutumia vizuri nafasi alizozipatakupachika mabao yaliyoipa Stars ushindi wa magoli 2-0 kwenye uwanja wa nyumbani.
“Magoli mawili niliyofunga kwenye timu ya taifa yataniongezea kujiamini na kwenda kufanya vizuri kwenye klabu yangu lakini nitaendelea kuaminika kwenye timu kwa sababu unapocheza kwenye timu ya taifa na kufunga wanaona huyu mchezaji anaweza kutusaidia,” Simon Msuva.

No comments:

Post a Comment