tuwasiliane

Sunday, February 5, 2017

Lipuli FC imerejea VPL 2017-18

LIPUL FC ya mkoani Iringa imerejea ligi kuu Tanzania bara baada ya kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Polis Dar na kufikisha alama 29 ambazo haziwezi lufikiwa na timu yeyote kwenye kundi lao la ligi Daraja la Kwanza.
Klabu hiyo kongwe ambayo inanolewa na kocha Richard Amatri, ilianza safari yake vizuri yenye matumaini kurejea Ligi Kuu Tanzania  Bara msimu ujao kwa kufanya vizuri katika mzunguko wa kwanza katika Kundi A.
Akizungumza na mtandao mmoja wa michezo nchini, kocha wa lipuli Richard Amatri amesema mia yao ilikuwa nikurejea ligi kuu nakufanya mapindunzi ya soka katika mkoa wao wa Iringa, hivyo wanajipanga ili wasishuke daraja tena.
“Mashabiki wetu waendelee kutusapoti na kamwe hatuwezi kuwaangusha tutajituma kadri ya uwezo wetu ili kuwapa matokeo mazuri kama tulivyokuwa tunafanya huku katika ligi daraja la Kwanza”, alisema Amtri.
Aidha kocha huyo amewapongeza viongozi wa Lipuli na wachezaji kwa juhudi walizozionesha kuanzia mwanzo msimu mpaka leo huku wakijivunia umoja waliokuwa nao katika timu yao ndiyo umezaa matunda.
Lipuli inaongoza kundi hilo ikiwa na alama 29  huku ikibakiwa na michezo miwili mikononi mwao.

No comments:

Post a Comment