tuwasiliane

Saturday, February 6, 2016

LIGI KUU YA VODACOM KUENDELEA WIKIEND HII

VPL R18
Ligi Kuu ya Vodacoma Tanzania bara raundi ya 18 inatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo nane kuchezwa katika viwanja mbalimbali nchini,Leo Jumamosi ukichezwa mchezo mmoja na kesho Jumapili kuchezwa kwa michezo saba.
leo Jumamosi ligi ya kuu ya Vodacom itaendelea kwa mchezo mmoja tu, ambapo katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, African Sports watawakaribisha Stand United kutoka mkoani Shinyanga.
Michezo saba itachezwa kesho siku ya Jumapili ambapo maafande wa JKT Ruvu watakuwa wenyeji wa Young Africans katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Mbeya City dhidi ya Tanzania Prisons uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, na Ndanda FC watawakaribisha Mtibwa Sugar katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Kagera Sugar watacheza dhidi ya Simba SC katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, Azam FC watawakaribisha Mwadui FC uwanja wa Chamazi, Majimaji dhidi ya Mgambo uwanja wa Majimaji mjini Songea na Toto Africans watawakaribisha Coastal Union uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

No comments:

Post a Comment