tuwasiliane

Wednesday, December 23, 2015

Mapinduzi cup kutimua vumbi Januari 2

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka visiwani Zanzibar Kassim Haji Salum amesema Klabu za Gor Mahia ya kenya , KCCA ya Uganda , Yanga, Simba, Azam FC na Mtibwa sugar kutoka Tanzania Bara na Mafunzo na JKU kutoka visiwani Zanzibar ndio Timu zitakazoshiriki Mashindano ya Mapinduzi Cup Mashindano ambayo yanatarajiwa kuanza Januari 2 visiwani Humo.
Michuano ya Mapinduzi Cup itazisaidia Timu za Yanga, Azam FC, JKU na Mafunzo kujiandaa na Mashindano ya CAF ya Klabu Barani Afrika.
Yanga watacheza michuano ya CAF Champion Ligi kwa kucheza mchezo wa mtoano na Timu ya Cercle de Joachim ya Mauritius wakati Azam FC watacheza na Mshindi kati ya Klabu ya Seychelles na Bidvest Wits ya Afrika Kusini katika Kombe la Shirikisho.
Mafunzo ya zanzibar wao watacheza na klabu ya AS Vita ya Congo DR kwenye CAF Champion Ligi na Timu ya JKU itashiriki Kombe la Shirikisho pamoja na Gaborone United ya Botswana.

No comments:

Post a Comment