tuwasiliane

Sunday, August 3, 2014

SHIRIKA LA NDEGE LA EMIRATES LASITISHA SAFARI ZA GUINEA

Ndege ya Emirates

Shirika la Ndege la Falme za Ghuba, Emirates, lenye makao yake Dubai, limesimamisha kwa muda safari za ndege za kwenda Guinea kwa sababu ya ugonjwa wa Ebola ambao umeuwa zaidi ya watu 700 Afrika magharibi mwaka huu.
Katika tovuti yake Emirates imesema haiwezi kutia hatarini afya ya abiria na wafanyakazi wake.
Ijumaa, Margaret Chan, mkurugenzi wa shirika la afya duniani, WHO, alisema virusi vya Ebola vinatapakaa haraka zaidi kushinda juhudi za kuvidhibiti.
Homa ya Ebola ilianza Guinea na kutapakaa nchi jirani za Sierra Leone na Liberia.
Mashirika mawili ya ndege ya Afrika, (Arik Air, ya Nigeria, na ASKY ya Togo,) yameshatangaza kuwa yamevunja safari za kwenda nchi zilizoathirika.
Shirika la ndege la Emirates halina safari za kwenda Sierra Leone au Liberia.

No comments:

Post a Comment