Kocha wa Brazil , Luiz Felipe Scolari, amesema kuwa
mshambulizi nyota wa Barcelona ya Uhispania na Brazil Neymar alikumbwa
na mshtuko na kuhofia kuwa alikuwa amepooza miguu yake punde baada ya
kugongwa uti wa mgongo na kiungo wa Colombia Juan Zúñiga .
Daktari wa timu hiyo Rodrigo Lasmar amedhibitisha kuwa Neymar amejeruhi uti wake wa mgongo na kuwa hatoweza kucheza kwa kipindi cha majuma manne hadi 6 yajayo .
Kauli hiyo imemlazimi Scolari kupanga upya safu yake ya mashambulizi ilikufidia pengo aliyoiwacha Mshambulizi huyo machachari.
Neymar alikimbizwa hospitalini kwa helikopta timu yake ilipokuwa ikiongoza 2-1 dhidi ya Colombia katika mechi ambayo wenyeji hao walijikatia nafasi ya nusu fainali dhidi ya Ujerumani.
Picha za mshambulizi huyo akilia ziliwatamausha mashabiki wake kote duniani .
Mashabiki wa Brazil sasa wamesalia na hofu kubwa kutokuwepo kwake huenda ikaifanya selecao kuwa wadhaifu mbele ya Ujerumani timu hizo zitakapokutana sikua ya jumanne.
Scolari amesema kuwa ''Bila shaka tumempoteza mchezaji ambaye anaweza kuleta tofauti kubwa mno katika mechi yeyote ile hususan katika mechi hiyo ya jumanne dhidi ya Ujerumani''
chanzo;bbc
No comments:
Post a Comment