tuwasiliane

Tuesday, July 1, 2014

ARGENTINA YAIPIGA USWISI 1-0 NA KUFUZU ROBO FAINALI

Embrace: Lionel Messi was the architect of the goal
 
ZIKIWA zimesalia dakika mbili mchezo kuhamia kwenye mikwaju ya penalti baada ya Argentina na Uswisi kuwa hazijafungana katika mchezo wa 16 Bora Kombe la Dunia jioni hii Brazil, Angel di Maria alifanya mambo.  
Nyota huyo wa Real Madrid aliitendea haki pasi nzuri ya Lionel Messi wa Barcelona dakika ya 118 kuipeleka Argentina Robo Fainali ya Kombe la Dunia.
Tofauti na ilivyotarajiwa akina Messi wangefuzu kiulaini, Uswisi waliibana Argentina na ilibaki kidogo mshindi aamuliwe kwa matuta.   
Kikosi cha Argentina kilikuwa; Romero, Federico Fernandez, Zabaleta, Garay, Rojo/Basanta dk105+1, Gago/Biglia dk106, Mascherano, Di Maria, Higuain, Messi na Lavezzi/Palacio dk74.
Uswisi; Benaglio, Lichtsteiner, Schar, Djourou, Rodriguez, Inler, Behrami, Xhaka (Fernandes 66), Shaqiri, Mehmedi/Dzemaili dk113 na Drmic/Seferovic dk82.

No comments:

Post a Comment