tuwasiliane

Monday, June 30, 2014

WACHEZAJI WALIOPIMWA WA COSTA RICA HAWANA TATIZO


Wachezaji saba wa Costa Rica waliolazimishwa na maafisa wa FIFA kupimwa mkojo punde baada ya ushindi wa kihistoria dhidi ya Italia wamedhibitishwa kuwa hakutumia dawa za kuongeza nguvu mwilini.
Maafisa wa Afya na wale wa kuchunguzi utumiaji wa madawa ya kututumua misuli yaliyopigwa marufuku walliwavamia wachezaji punde baada ya ushindi huo mkubwa na kuwatenga hadi pale walipochukua mkojo kwa ajili ya kupima chembe chembe za damu .
Tukio hilo lilikuwa la kustaajabisha kwani timu hiyo ilikuwa baadhi ya timu zilizokuwa zimeshukiwa kutokana na mchezo wao mzuri.
Awali wachezaji kadha walilazimika kupimwa punde baada ya mechi ambayo Costa Rica iliizaba Uruguay mabao 3-1.

Mfumo huu wa kupima mkojo wa wachezaji punde baada ya mechi imeiwacha FIFA ikishtumiwa kwa kupendelea timu fulani kushamiri katika kombe la dunia huku timu ambazo hazikutarajiwa kunawiri zikishurutishwa kupimwa dawa za kututumua misuli zilizopigwa marufuku.

Aliyekuwa mchezaji wa wa Argentina Diego Maradona aliiunga shirikisho la soka la Costa Rica kuikashifu FIFA akisema mbinu hiyo mpya inalenga kuwazonga wachezaji na mawazo kabla ya kipute hicho kumalizika nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment