tuwasiliane

Monday, June 23, 2014

URENO YAJIWEKA PABAYA,YATOKA SARE 2-2 DHIDI YA MAREKANI

 


Ureno ambayo ilikuwa imepata pigo kubwa iliposhiindwa katika mechi yake ya ufunguzi na Ujerumani na ilikuja katika mechi hii ikitafuta ushindi wa aina yeyote ilikuepuka fedheha ya kufungashwa virago katika hatua ya makundi katika kombe la dunia linaloendelea huko Brazil.
Kwa upande wao Marekani, ilikuwa inafahamu fika kuwa matokeo baina ya 2-2 naina ya Black Stars ya Ghana na vinara wa kundi G Ujerumani ilikuwa na hatari ya kuinyima fursa ya kushiriki mkondo wa pili wa kombe la dunia kwa hivyo ilikuwa inatafuta ushindi ambao ingeipa tiketi ya moja kwa moja katika hatua ijayo.
Lakini kipenga cha kuanza kwa mechi hii kilpopulizwa, Nani ndiye aliyeiweka Ureno mbele baada ya dakika 5 ya mechi hiyo.

Kuanzia hapo nipe nikupe baina ya mahasimu hao wa jadi ikaendelea hadi dakika ya 64 Germaine Jones alipofaidi safu tepetevu ya ulinzi na kuisawazishia Marekani.
Vijana wa Jurgen Klinsmann ndiyo walionekana na tamaa zaidi ya kushiriki mkondo wa pili wa kombe la dunia walipofaidi kona iliyotokana na makosa ya Ricardo Costa
na wakaitumia vyema.
Marekani ilifufua matumaini ya kusonga mbele Clint Dempsey alipovurumisha mkwaju ndani ya neti na kuiweka timu yake mbele , hata hivyo Christiano Ronaldo alimwandalia pasi nzuri na akaisawazishia Ureno katika muda wa ziada wa mechi hiyo.

Mwisho wa kuishia Ureno ilijizolea alama yake ya kwanza katika kipute hicho huko Brazil lakini wanahitaji kuilaza Ghana na kuomba kuwa Marekani wakunguwae dhidi ya ujerumani iliwao wafuzu kusonga mbele.
Marekani inahitaji ushindi mkubwa dhidi ya Ujerumani ambayo itakuwa ikitafuta sare ya aina yeyote ilikusonga mbele.
Ghana kwa upande wao sasa wanahitaji kuichapa Ureno na kuomba kuwa Ujerumani nayo itaitandika Marekani iliwafuzu kwa mkondo ujao.
Kufikia sasa ujerumai inaongoza kundi hili ikiwa na jumla ya ponti 4 sawa na Marekani.Ghana ni ya 3 na alama 1 sawa na Ureno .

No comments:

Post a Comment