tuwasiliane

Monday, June 30, 2014

ROBEN AKIRI KUJIANGUSHA

 



Mshambulizi wa Uholanzi Arjen Robben amekiri kuwa alidanganya timu yake ikapewa penalti ya ushindi lakini akasema alikuwa ametegwa .
Kocha wa Mexico Miguel Herrera amemkashifu refarii wa mechi yao na Uholanzi Pedro Proenca kwa kuipendelea Uholanzi .
Herrera amesema kuwa Penalti hiyo dakika tatu kabla ya kukamilika kwa mechi hiyo haikufaa''hiyo ni njama ya FIFA kuiondoa Mexico kwenye kinyang'anyiro hicho .
Robben alikunguwa katika eneo la lango Uholanzi ilipokuwa imesawazisha bao moja kwa moja na ikaisaidia Uholanzi kuibuka mshindi kwa mabao 2-1 .

“nataka kwanza kuwaomba radhi mashabiki wangu kwa kudanganya na kujiangusha ukweli haikufaa '' Robben aliiambia runinga ya Uholanzi NOS.

''nafikiri kuwa refarii Proenca alifanya kweli kuashiria penalti akisema kuwa alikuwa ametegwa na nahodha wa Mexico Rafael Marquez.
Mexico ilikuwa imeongoza hadi dakika ya 88 ya kipindi cha pili kabla Wesley Sneijder kuisawazishia Uholanzi kabla ya Huntelaar kufunga penalti iliyozua ubishi mkubwa.
Herrera alisema kuwa haikufaa refarii kutoka ulaya alipewa mechi kati ya timu kutoka ulaya na Marekani ya kusini.
Kwanini FIFA hawakutupa refarii mwafrika mhindi ama hata refarii kutoka Marekani kusini ?

No comments:

Post a Comment