POLE YA DOCTA SLAA KWA WATU WA ARUSHA
Wana Arusha,
Kwa masikitiko makubwa, Mimi na mama Slaa tumepokea tukiwa Munich
Ujerumani kwa masikitiko makubwa tukio la kulipuliwa Bomu katika mkutano
wa Kampeni ya uchaguzi mdogo wa Madiwani, Arusha.
Tunatoa pole kwa familia zote za waliopoteza maisha katika tukio Hilo
na pia tunamwomba kwa namna ya pekee Mwenyezi Mungu awape faraja wote
walioumia kwa namna mmoja au nyingine na kuwapa faraja na neema kubeba
maumivu waliyopata.
Chadema tunaanza na Mungu, tunaendelea na
Mungu na tunamaliza na Mungu. Kama mtu asiye na dhamira na ubinadamu,
awaye yeyote, na kwa sababu yeyote ile amefanya hivyo, katika hatua hii
ni Imani yangu kuwa Damu ya ndugu zetu hao haitapotea bure. Kwa damu
hiyo watanzania tushikamane zaidi, kuwaombea waliotutangulia mbele ya
haki, lakini damu hiyo ituunganishe zaidi katika kupigania Tanzania
isiyo na maonevu ya aina yeyote ile.
Hali hii sasa haivumiliki
tena. Nchi inayoyoma, na hatuwezi kuendelea kutazama nchi inaporomoka.
Tukiisha kutoa tahadhari miaka miwili iliyopita hawakutusikiliza. Hakuna
Maisha ya Mtanzania hata mmoja kupotea katika mazingira yanayopaswa
kuwa ya Amani. Uchaguzi kimsingi unapaswa kuwa tukio la Amani. Jukumu la
kuhakikisha Amani ni la serikali na hakuna sababu ya kigugumizi
Serikali inaposhindwa kutimiza wajibu wake wa msingi.
No comments:
Post a Comment