
Askofu Mkuu wa Kanisa la Good News For All Ministry, Charles Gadi PICHANI, kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali wa dini, leo wameandaa ibada maalumu ya maombi ya wazi ya timu ya Taifa, ‘Taifa Stars’ ili iweze kuibuka na ushindi kwenye mchezo dhidi ya Ivory Coast kesho kwenye Uwanja wa Taifa.
Gadi aliwataka Watanzania kuungana pamoja kuiombea timu hiyo, kwani haijawahi kufika mbali katika mchezo ya kimataifa.
“Tuna imani timu yetu ni nzuri, lakini inahitaji maombi zaidi kwa kuwa inacheza na timu ngumu,” alisema askofu Gadi.
Aliitaka jamii iendelee kufanya maombi na kuhamasisha misaada ya hali na mali kwa timu hiyo.
Wakati huohuo, Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen
amewapa wachezaji wake mbinu mpya ya kuwakabili nyota wa Ivory Coast
katika mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu Kombe la Dunia mwakani nchini
Brazil.
Poulsen alisema kubwa alilowafundisha wachezaji
wake ni kujiamini watakapokuwa wakicheza na miamba hiyo ya soka Afrika.
“Nimewaambia wachezaji wajiamini, wasicheze na majina ya wapinzani
wao,” alisema Poulsen.
“Ivory Coast ni timu bora, lakini nimewataka
wachezaji wangu waione kama timu ya kawaida kwenye mchezo wa Jumapili.
Jambo la msingi wacheze kwa kujiamini,” alisema Poulsen.
No comments:
Post a Comment