tuwasiliane

Friday, June 14, 2013

Cecafa yaziba pengo la Yanga, Simba





Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa), imeziteuwa timu ya Mamlaka ya Mapato Uganda (URA), Elect Sports ya Chad na Rayon Sports ya Rwanda kuziba nafasi ya timu za Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Kagame inayoanza Juni 18-Julai 2, Sudan.
Simba, Yanga na Falcon ya Zanzibar hazitashiriki michuano hiyo kwa maagizo ya serikali kutokana na mashaka ya usalama nchini Sudan hasa kwenye Jimbo la Darfur ambalo ni moja ya kituo cha mashindano.
Katibu Mkuu wa Cecafa Nicholaus Musonye alisema kujiondoka kwa timu za Tanzania, kusingekuwa mwisho wa mashindano hayo kwa vile baraza hilo lina timu nyingi.
“Tumeziteua timu hizi baada ya ushawishi wetu kwa timu za Tanzania kushiriki kushindikana,” alisema Musonye na kuongeza sababu zilizotajwa na Tanzania kutokushiriki michuano hiyo hazina mashiko.
Alisema wanatarajia kupanga upya ratiba ya michuano hiyo katika mkutano wa wajumbe wa Cecafa na waandaaji utakaofanyika mjini Khartoum.
Musonye alilaumu mwingilio wa mashindano hayo na mambo ya siasa kama ilivyotokea mwaka huu.

No comments:

Post a Comment