tuwasiliane

Wednesday, March 27, 2013

SIMBA YAZIDI KUUWEKA UBINGWA REHANI,AZAM YATAKATA

MNYAMA chali Kaitaba. Naam, Wekundu wa Msimbazi leo wameshindwa kufurukuta mbele ya Kagera Sugar, baada ya kuchapwa bao 1-0 kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba jioni hii.

Matokeo hayo yanzidi kupoteza matumaini ya Simba SC japo kucheza michuano ya Kombe  la Shirikisho Afrika mwakani, wakiwa wanazidiwa pointi sita sasa na Azam FC (40-34) inayoshika nafasi ya pili.
 Yanga inaongoza kwa pointi zake 48. 
Hadi mapumziko hakuna timu iliyokuwa imefanikiwa kupata bao na Kagera Sugar ndio waliocheza vizuri zaidi na kukaribia kufunga mara mbili. 

Kwanza ilikuwa dakika ya tano, baada ya Jumanne Daudi kumjaribu ‘Tanzania One’, Juma Kaseja lakini shuti lake likapaa juu ya lango na baadaye dakika ya 22 Juma Nade alitaka kutumia vema makosa ya beki Shomary Kapombe kuchelewa kuokoa, lakini akapiga fyongo.

Kipindi cha pili Kagera Sugar inayofundishwa na gwiji wa zaman wa SImba SC, ABdallah Kibadeni, iliingia na kasi  ya kutosha na kufanikiwa kupata bao la mapema tu dakika ya kwanza.  

Alikuwa ni beki Amandus Nesta aliyefanikiwa kufunga bao hilo dakika ya 46 akiunganisha kwa kichwa kona iliyochongwa na beki wa zamani wa Simba SC, Salum Kanoni Kupela. 
Simba SC; Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Miraj Adam, Hassan Khatibu, Shomary Kapombe, Jonas Mkude, Edward Christopher, Abdallah Seseme, Mrisho Ngassa, Ramadhan Singano ‘Messi’ na Haruna Chanongo.
Kagera Sugar; Andrew Ntala, Benjamin Asukile, Salum Kanoni, Benjamin Effe, Amandus Nesta, Malegesi Mwangwa, Juma Mpola, Juma Nade, Jumanne Daudi, Darington Enyinna na Paul Ngway.
wakati huo huo, katika uwanja wa chamanzi 
AZAM FC imejiweka sawa katika kuifukuza Yanga SC kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya jioni hii kuilaza mabao 3-0 Prisons ya Mbeya kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo, Azam imefikisha pointi 40 na kubaki inazidiwa pointi nane na Yanga SC.
Tchetche akifunga

Hadi mapumziko, tayari Azam walikuwa mbele kwa bao 1-0 lililowekwa nyavuni na mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche dakika ya 17.
Tchetche alifunga bao zuri, baada ya kupokea pasi ya Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na kuambaa pembezoni upande wa kushoto mwa Uwanja akiingia ndani, kama anataka kupiga krosi lakini akaunganisha mwenyewe nyavuni kwa shuti kali la kushitukiza. 
Azam ingeweza kupata mabao mawili zaidi kipindi cha kwanza kama ingekuwa makini kutumia nafasi ilizozitengeneza.
Prisons walicheza vizuri na walikaribia kufunga mara mbili kwa mashambulizi ya kutokea upande wa kushoto mwa Uwanja. 
Kipindi cha pili, Azam walirejea na kasi zaidi na kufanikiwa kupata mabao mawili zaidi, yaliyofungwa na John Raphael Bocco ‘Adebayor’ dakika ya 76 na Tchetche tena dakika ya 84.
Katika mchezo huo, kikosi cha Azam FC kilikuwa; Mwadini Ally, Himid Mao, Waziri Salum, Luckosn Kakolaki, Joackins Atudo, Kipre Balou, Kipre Tchetche, Salum Abubakar/Ibrahim Mwaipopo, John Bocco, Humphrey Mieno/Abdi Kassim ‘Babbi’ na Khamis Mcha ‘Vialli’.
Priosns FC; David Burhan, Aziz Sibo/Henry Mwalugala, Laurian Mpalule, Lugano Mwangama, Jumanne Elfadhil, Nurdin Issa, Jeremiah Mgunda, Khalid Fupi, Elias Maguli, Freddy Chudu/ Peter Kizengele na Ramadhani Katamba/Hamisi Mango.

No comments:

Post a Comment