tuwasiliane

Wednesday, December 12, 2012

Hayatou kuchaguliwa bila kupingwa


Issa Hayatou
Issa Hayatou Rais wa CAF

Rais wa shirikisho la mchezo wa soka barani Afrika, CAF, Issa Hayatou, anaelekea kushinda awamu nyingine ya kuliongoza shirikisho hilo bila kupingwa, katika uchaguzi mkuu ujao.
Baada ya mkutano wa kamati kuu ya CAF uliofanyika tarehe 10 Desemba mwaka huu, katibu mkuu wa shirikisho hilo alilifahamisha kamati hiyo kuwa Hayatou, ndiye mgombea wa pekee katika kiti cha urais.
Afisa mkuu wa shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA Jacques Anouma, alikuwa ametangaza kuwa atawania kiti hicho katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mjini Maraketch, nchini Morocco mwezi Machi mwaka ujao.
Anouma kutoka Ivory Coast alitoa tangazo hilo, licha ya kufahamu kuwa kwa mujibu wa sheria za CAF, hangeliruhisiwa.
Hayatou, mwenye umri wa miaka 66, aliongoza mikakati ya kubadili katiba ya CAF, ambayo sasa inaruhusu wanachama wake wa kamati kuu pekee walio na haki ya kupiga kura, kuwania kiti cha urais.

Hayatou adaiwa kubadili sheria kujinufaisha

Anouma ni mwanachama wa kamati kuu ya CAF, kwa kuwa yeye ni muakilisha wa bara la Afrika katika kamati kuu ya FIFA.
Jacques Anouma
Jacques Anouma mwanachama wa kamati kuu ya FIFA

Licha ya kuwa yeye huhudhuria mikutano ya kamati kuu ya CAF, hana haki ya kushiriki katika zoezi lolote la kupiga kura.
Jina na Anoumaa linaaminika kuwasilishwa kwa kamati kuu ya CAF, kabala ya tarehe siku ya mwisho ya kuwasilisha maombi, lakini kwa sasa haliko katika, orodhaa ya majina ya watu wanaowania viti mbali mbali, kwa mujibu wa orodha iliyochapishwa kwenye mtandao wa CAF.
Juhudi za Liberia za kutaka sheria hiyo kubatilisha ziligonga mwamba pale ombi lao lilipotupiliwa mbali na mahakama ya upatinishi ya michezo CAS, kwa misingi kuwa Liberia haikuwa imefuata sheria zote za CAF, kutatua mzozo huo.
Rais wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Liberia, Hassan Musa Bility, ambaye aliomgoza uasi huo, ni miongoni mwa wale watakaowania nafasi katika kamati kuu ya CAF.
Danny Jordaan, kutoka Afrika Kusini ambaye, kwa mujibu wa sheria za sasa hawezi kuwania kiti cha urais, atawania kuwa muakilisha wa kanda ya Afrika Kusini katika kamati kuu ya CAG.

No comments:

Post a Comment