tuwasiliane

Saturday, June 16, 2012

16 JUN. MATOKEO YA MICHEZO YA JANA YA EURO 2012


FRANCE 2 UKRANE 0
Ufaransa ilipata ushindi wake wa kwanza katika kundi D katika mechi ya Ijumaa ya Euro 2012, baada ya kuwashinda wenyeji Ukraine katika uwanja ulioloa maji kufuatia mvua kubwa katika uwanja wa Donetsk.

Mchezo ulisitishwa baada ya dakika nne tu, kufuatia uwanja kuloa, na timu zilirudi uwanjani baada ya saa nzima kupita.

Lakini waliporudi, kulikuwa hakuna njia nyingine ya kuiokoa Ukraine, kuanzia wakati Jeremy Menez, mchezaji wa St Germain ya Ufaransa, alipowaongoza Wafaransa katika kufunga mabao, akitumbukiza mpira kutoka yadi 12.

Yohan Cabaye alifunga bao la pili.

Hilo lilikuwa ni bao la kwanza katika mechi ya kimataifa kwa mchezaji huyo wa klabu ya Newcastle inayocheza katika ligi kuu ya England.

Bao hilo lilipatikana kwa urahisi kufuatia kosa la wachezaji wa ulinzi wa Ukraine namna walivyocheza katika uwanja huo wa Donbass Arena.

Wachezaji wa timu zote walikuwa na kibarua kigumu katika kucheza katika hali ya joto kali na uwanja ulioloa, na ndio maana mwamuzi Bjorn Kuipers kutoka Uholanzi awali alikuwa ameamua kusitisha mechi hiyo.

Ilibidi juhudi za dharura kufanyika ili kuyafyonza maji hayo, na baadaye mwamuzi kuidhinisha mechi kuendelea.

katika mchezo mwingine
Danny Welbeck aliweza kuandikisha bao la ushindi la England dhidi ya Sweden, katika mechi ya kusisimua ya kundi D.

England iliweza kutangulia kwa bao la kwanza wakati Andy Caroll alipofunga kwa kichwa, baada ya kuletewa mpira wa juujuu kutoka kwa Steven Gerrard.

Lakini mlinzi Olof Mellberg aliweza kufunga bao la kusawazisha, na baadaye kupata la pili kwa kichwa na kuiwezesha Sweden kuongoza kwa mabao 2-1.

Mchezaji wa zamu Theo Walcott kupitia mkwaju kutoka yadi 25 aliiwezesha England kusawazisha, na kisha baadaye alipompigia mpira Welbeck, akafanikiwa kufunga bao la tatu na la ushindi, na kuhakikisha Sweden wanaelekea nyumbani baada ya kuwaondoa katika mashindano ya mwaka huu ya Euro 2012.

Huu ndio ushindi mkubwa zaidi wa England dhidi ya timu ya Sweden, na mara tu baada ya Carroll kuwawezesha kuongoza, England haikuona tena kitisho kikubwa mno cha kulemewa katika mechi hiyo ya Ijumaa.

Pengine onyo la nahodha Steven Gerrard kabla ya mechi katika kuhakikisha mshambulizi Zlatan Ibrahimovic asipate nafasi za kufunga labda ziliweza kuisaidia England kuepuka kushindwa.

Lakini kwa kumzuia Ibrahimovic, pengine ndio maana mchezaji mwenzake Melberg alipata bao la pili la Sweden kwa urahisi kwa kuwa England hawakumzuia kikamilifu.

Meneja wa England Roy Hodgson kisha aliamua kumtumia Walcott, na bila shaka mchezaji huyo alibadilisha mchezo.
Habari Muhimu

No comments:

Post a Comment