
Mashindano ya mchezo wa mpira wa miguu ya Mataifa ya Ulaya, Euro 2012 yameanza rasmi nchini Poland, moja ya nchi zinazoshirikiana kuandaa mashindano ya mwaka huu.
Katika mechi ya ufunguzi Dimitris Salpigidis alirudisha bao katika kipindi cha pili kusawazisha bao la mwenyeji wake Poland lililopatikana katika kipindi cha kwanza.
Mshambuliaji huyo aliwaudhi mashabiki wa Poland waliotazamia kuanza mashindano waliyoyaandaa wenyewe kwa kutikisa nyavu za Poland katika dakika ya 51, dakika 6 baada ya kipindi cha pili kuanza.
Hadi mapumziko, Robert Lewandowski anayetazamiwa kujiunga na Klabu ya Ligi ya England, Manchester united msimu ujao alikua ameisha ipatia Poland bao la kwanza katika dakika ya 17 ya mchezo.
Timu hizi mbili zilimaliza mechi zikiwa na wachezaji 10 kila upande na Ugiriki itajilaumu kwa kupoteza fursa wazi ya kuongoza kupitia mkwaju wa peneti baada ya Giorgos Karagounis kukosa peneti hio kufuatia kosa la kipa wa Poland Wojciech Szczesny kusababisha aondolewe kwa kadi nyekundu kwa kumuangusha Salpigidis katika eneo la hatari mnamo dakika ya 69th.
Kabla ya hapo beki wa Ugiriki Sokratis Papastathopoulos alikua mchezaji wa kwanza kwenye mashindano haya ya Euro kuonyeshwa kadi nyekundu, baada ya kupokea kadi mbili za njano mnamo dakika ya 35 na 44.
Hivi sasa timu hizi zina pointi 1 kila moja.
katika mchezo wa pili jana
Urusi ilionyesha ustadi mkubwa ilipocheza na Jamhuri ya Czech katika mechi ya pili ya Euro 2012 siku ya Ijumaa, na mabao mawili ya Alan Dzagoev kuisaidia kuwaangamiza wapinzani wao katika siku ya kwanza ya mashindano hayo.
Dzagoev aliiwezesha Urusi kupata bao la kwanza, huku Roman Shirokov akiandikisha la pili, baada ya Andrey Arshavin kumuandalia mpira huo.
Vaclav Pilar aliweza kuifungia Jamhuri ya Czech bao moja, na kupunguza tofauti ya mabao kati ya timu hizo mbili.
Lakini ilielekea kana kwamba bao hilo la Czech liliamsha gadhabu za Warusi, na ambao pasipo kusubiri sana, Dzagoev aliweza kutumbukiza magoli mawili zaidi, na mchezaji wa zamu Roman Pavlyuchenko naye akiandikisha lake pia.
Ilikuwa dhahiri kwamba Urusi ndio iliyokuwa timu bora katika uwanja wa Wroclaw, na Jamhuri ya Czech ikionyesha udhaifu mkubwa nchini Poland.
Kocha wa Czech, Michel Bilek bila shaka atakuwa na kibarua kigumu katika kuwahimiza wachezaji wake waliovunjika moyo kwamba bado wanaweza kujikakamua na kufanya vyema watakapokutana na Ugiriki tarehe 12 Juni.
Hii itakuwa ni mechi muhimu kwa Czech, ikiwa ina nia ya kuendelea na mashindano ya Euro.
Kutokana na wenyeji Poland kumaliza mechi ya ufunguzi dhidi ya Ugiriki kwa sare ya 1-1, timu ya Urusi na Czech walianza mechi yao wakifahamu kwamba mshindi katika pambano lao ataweza kuwa kileleni katika kundi lao.
Urusi, ambao chini ya meneja Guus Hiddink waliweza kufika nusu fainali katika mashindano ya mwaka 2008, na kuonyesha kwamba hawana utani katika michuano ya mwaka huu.
No comments:
Post a Comment