Klabu ya watoto wa Jangwani Dar Young Africans, imewatupia virago beki wake wa kulia na nahodha, Shadrack Nsajigwa ‘Fuso’ na Abuu Ubwa, imefahamika.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya klabu hiyo yenye maskani yake makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Kariakoo, jijini Dar es Salaam zinasema, nyota hao wameachwa kutokana na kushuka viwango.
Chanzo cha uhakika kimedokeza kuwa kushuka kwao kiwango kuliwafanya washindwe kutoa mchango uliotarajiwa kutoka kwao katika msimu uliopita wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara iliyofikia tamati Mei 6.
Yanga chini ya Kocha wake Mserbia, Kostadin Papic ilimaliza ligi hiyo kwa kushindwa kutetea ubingwa wake, ikimaliza nafasi ya tatu nyuma ya Simba na Azam FC.
Chanzo hicho kimedokeza kuwa, kuachwa kwa nyota hao, ni sehemu ya mkakati wa kukisuka upya kikosi cha timu hiyo kuelekea vita ya kutetea ubingwa wa Kombe la Kagame na msimu mpya wa Ligi Kuu.
Mbali ya kiwango, pia kiongozi huyo amedokeza kuwa, walikerwa na utovu wa nidhamu wa ndani na nje ya uwanja wa Nsajigwa aliyekuwa nahodha wa timu ya soka ya Tanzania, T
No comments:
Post a Comment