
MTANZANIA Nelly Kamwelu ameshika nafasi ya tano katika shindano la Miss Tourism Queen International 2011/12, lililofanyika katika mji wa Xian, nchini China.
Kamwelu alikuwa akiiwakilisha Tanzania katika shindano hilo baada ya kuibuka mshindi wa Miss Universe Tanzania mwaka huu.
Nelly ameshika nafasi hiyo mbele ya warembo wengine 92 katika shindano hilo ambalo ni la 5 kwa ukubwa duniani linalohusu mamiss.
Taji hilo la Miss Tourism Queen International, lilichukuliwa na mrembo wa kutoka nchini Thailand.
Nelly anatarajiwa kurejea nchini leo kwa ndege ya shirika la Emirates.
No comments:
Post a Comment