
Aliweza kukiri kwamba timu yake bado haijafikia kiwango wanachokitaka na kwamba hali hiyo ndiyo iliyowafanya wazidiwe na kulala 2-0, kwenye mechi yao ya kirafiki dhidi ya Azam iliyochezwa juzi kwenye Uwanja wa Taifa hapa Jijini.
Si mwingine bali ni yule Kocha wa Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Kostadin Papic kwamba mechi hiyo imempa picha kwamba bado wachezaji wake hawajafikia kiwango cha kukabiliana na ushindani dhidi ya timu zenye maandalizi ya kutosha.
Alisema kikosi chake chahitaji dozi zaidi ya mazoezi ili wafikie katika ubora wanaouhitaji.
Ndani ya mechi hiyo watoto wa Jangwani waliburuzwa kwa kasi ya ajabu, kwa pasi maridadi za Azam katika muda mwingi wa mechi na hivyo.
Kwani hakukuwa na shabiki aliyeshangaa kuona wakipata kipigo kilichotokana na mabao hayo kutoa kwa washambuliaji hao wa zamani yaani Gaudence Mwaikimba aliyefunga la utangulizi katika kipindi cha kwanza na Mrisho Ngassa aliyeongeza jingine katika kipindi cha pili.
Papic, alisema kuwa mechi hiyo imempa picha kwamba bado wachezaji wake hawajafikia kiwango cha kukabiliana na ushindani dhidi ya timu zenye maandalizi ya kutosha, hivyo wanahitaji 'dozi' zaidi ya mazoezi ili wafikie katika ubora wanaouhitaji.
Yanga na Azam watakutana tena mwezi ujao visiwani Zanzibar katika mashindano ya Kombe la Mapinduzi yatakayoanza Januari 2.
No comments:
Post a Comment