tuwasiliane

Saturday, December 12, 2015

Platini ashindwa rufaa ya kupinga marufuku

Platini
Rais wa Shirikisho la Soka Ulaya Uefa Michel Platini ameshindwa katika rufaa yake ya kutaka marufuku ya siku 90 dhidi yake iondolewe.
Alikuwa amewasilisha rufaa akitaka marufuku ya kutojihusisha na soka kwa miezi mitatu iondolewe kumuwezesha kuendelea na kazi lakini hilo limekataliwa na Mahakama ya Mizozo ya Michezo.
Platini, 60, alisimamishwa kazi pamoja na rais wa Fifa Sepp Blatter mwezi Oktoba huku uchunguzi wa madai ya rushwa dhidi yao yakiendelea kuchunguzwa.
Wote wawili wamekanusha tuhuma hizo.

No comments:

Post a Comment