Kocha wa Gor Mahia Bobby Williamson amechaguliwa kuwa
kocha wa Harambee Stars ya Kenya baada ya Adel Amrouche kufutwa kazi
siku ya Jumapili kufuatia kushindwa kwa Kenya katika raundi ya kwanza ya
mchujo dhidi ya Lesotho.
Hata hivyo raiya huyo wa Scotland amesema kuwa bado ataendelea na majukumu yake katika klabu mabingwa wa ligi kuu ya Kenya KPL hadi pale shirikisho la soka la Kenya FKF litakapokubaliana na klabu yake ya Gor Mahia.
Williamson anatarajiwa kuiongoza Gor mahia katika mchuano wa baraza la soka kanda ya Afrika Mashariki na Kati baada ya kutwaa taji la taifa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 18.
Kocha huyo Aliiambia BBC kuwa ni wakati shirikisho la soka la Kenya FKF lirejelee soka ya vijana chipukizi ilikuimarisha nafasi yake ya kuboresha matokeo yake kimataifa.
No comments:
Post a Comment