tuwasiliane

Saturday, July 5, 2014

BRAZIL YATINGA NUSU FAINAL YA WORLD CUP 2014,YAIPIGA COLOMBIA 2-1, NEYMAR AUMIZWA VIBAYA


Awali Thiago Silva alioneshwa kadi ya njano na hivyo hataweza kushiriki mechi ya nusu fainali dhidi ya Ujerumani siku ya jumanne .

 Brazil 2-1 Colombia: David Luiz wonderstrike sends hosts through as Neymar is stretchered off



Brazil imejikatia tikiti ya nusu fainali ya kombe la dunia baada ya kuilaza Colombia mabao 2-1 katika mechi ngumu ya robo fainali.
Kufuatia ushindi huo Brazil sasa watachuana na Ujerumani katika nusu fainali iliyoratibiwa kuchezwa Jumanne ijayo Julai tarehe 8.
Kama ilivyo tarajiwa vijana wa Luiz Felipe Scolari ambao ''wana mkono mmoja kwenye kombe la dunia kulingana na kocha huyo'' walitangulia kuweka niya yao wazi kunako dakika ya 7 ya kipindi cha kwanza Thiago Silva alipofunga kwa kichwa mkwaju ambao ulimwacha kipa machachari David Ospina asijue la kufanya .
Baada ya kipindi cha pili kwanza ,Colombia walikuwa mbioni wakitafuta bao la kusawazisha dhidi ya wapinzani wao waliofurahia umati wa nyumbani ,Ghafla bin vuu Brazil wakaongeza bao la pili kupitia kwa mkwaju wa Freekick wa David Luiz kunako dakika ya 69 ya kipindi hicho cha pili .

Kuanzia hapo Brazil ilianza kulinda ngome yake dhidi ya wimbi baada ya wimbi ya mashambulizi kutoka kwa Colombia.
Bao la kufutia machozi la Colombia lilipachikwa kimiani kupitia mkwaju wa penalti kipa wa Brazil Julio Cesar alipomwangusha James Rodriguez katika eneo la lango.
Rodriguez aliutia kimiani na kusajili bao lake la sita.
Mshambulizi huyo wa Colombia ndiye anayeongoza katika ufungaji mabao huko Brazil.


 Neymar ruled out of World Cup with broken vertebra
Taharuki ilitanda uwanjani na kwa ukumbwa Brazil nzima baada ya nyota wao Neymar kuondolewa kwa haraka uwanjani na kukimbizwa hospitalini baada ya kujeruhi uti wa mgongo na Juan Camilo Zuniga.

No comments:

Post a Comment