Awali Thiago Silva alioneshwa kadi ya njano na hivyo hataweza
kushiriki mechi ya nusu fainali dhidi ya Ujerumani siku ya jumanne .
Brazil imejikatia tikiti ya nusu fainali ya kombe la
dunia baada ya kuilaza Colombia mabao 2-1 katika mechi ngumu ya robo
fainali.
Kufuatia ushindi huo Brazil sasa watachuana na
Ujerumani katika nusu fainali iliyoratibiwa kuchezwa Jumanne ijayo Julai
tarehe 8.Baada ya kipindi cha pili kwanza ,Colombia walikuwa mbioni wakitafuta bao la kusawazisha dhidi ya wapinzani wao waliofurahia umati wa nyumbani ,Ghafla bin vuu Brazil wakaongeza bao la pili kupitia kwa mkwaju wa Freekick wa David Luiz kunako dakika ya 69 ya kipindi hicho cha pili .
Kuanzia hapo Brazil ilianza kulinda ngome yake dhidi ya wimbi baada ya wimbi ya mashambulizi kutoka kwa Colombia.
Bao la kufutia machozi la Colombia lilipachikwa kimiani kupitia mkwaju wa penalti kipa wa Brazil Julio Cesar alipomwangusha James Rodriguez katika eneo la lango.
Rodriguez aliutia kimiani na kusajili bao lake la sita.
Mshambulizi huyo wa Colombia ndiye anayeongoza katika ufungaji mabao huko Brazil.
Taharuki ilitanda uwanjani na kwa ukumbwa Brazil nzima baada ya nyota wao Neymar kuondolewa kwa haraka uwanjani na kukimbizwa hospitalini baada ya kujeruhi uti wa mgongo na Juan Camilo Zuniga.
No comments:
Post a Comment