tuwasiliane

Friday, June 27, 2014

MAXIMO ASAINI MIWILI YANGA















Kocha mbrazil Marcio Maximo leo amesaini mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuwatumikia Mabingwa mara 24 wa Ligi Kuu ya Vodacom timu ya Young Africans pamoja na msaidizi wake Leonadro Neiva ambao wamesema wamekuja kuisaidia Yanga iweze kufanya vizuri kwenye michuano mbalimbali.

Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga, Maximo amesema anajiskia furaha sana kurudi kufanya kazi Tanzania, kwani watu wake ni wakarimu, wapenda mpira hivyo anaona kama yupo nyumbani japo awamu hii ni kwa majukumu ya ngazi ya klabu tofauti na awali alipokua ngazi ya Taifa.
Nimekuja kufanya kazi na Yanga, nawashukuru viongozi wake kwa kuamua kuniamini na kunipa nafasi hii, wamenifuatilia kwa awamu tatu mfululizo na hatimaye safari hii wamefanikiwa kunipata kwa kushirikiana na wakala wangu Ally Mlei sasa kazi ni moja tu kuijenga Yanga.
"Jumatatu naanza kazi moja kwa moja pamoja na msaidizi wangu Neiva kwa kushirikiana na kocha wa kikosi cha U-20, wachezaji waliopo na wachezaji wa kikosi cha U20 watakua wakifanya mazoezi pamoja alisema" Maximo".

Natambua tuna wachezaji wengi katika timu za Taifa mbalimbali ikiwemo ya Tanzania (Taifa Stars), Uganda  (The Cranes) na Rwanda (Amavubi) ambao wapo wanayatumikia mataifa yao, na punde watakapomaliza majukumu hayo wataungana nasi kwa maandalizi.

Kuhusu Kaseja yale yalishapita, najua ni kipa mzuri mwenye uwezo na uzoefu wa kutosha na kipindi hiki najivunia kuwa na makipa watatu wenye uwezo mzuri, Yaliyopita Yameshapita yalikuwa ni timu ya Taifa na sasa tumekutana Yanga kazi yetu ni moja tu kuifanya klabu iwe kwenye hadhi ya Kimataifa zaidi.

Naye kocha msaidizi Leonado Neiva amesema tumekuja kufanya kazi, kwa kushirikiana na wachezaji waliopo kutoka sehem mbambali barani Afrika na Amerika tutapata mchanganyiko mzuri wa uchezaji.
Wakala wa Maximo Barani Afrika Bw Ally Mlehi kwa upande wake amewaomba wapenzi, wanachama na washabiki wa Yanga kuwa wavumilivu kwani soka ni tofauti ni chai ambayo ukikoroga sukari tu unasikia utamu, badala yake wanapaswa kuwapa muda makocha na baadae wataaona matunda yake.

source.www.http://youngafricans.co.tz

No comments:

Post a Comment