tuwasiliane

Wednesday, June 25, 2014

IVORY COAST YAPIGWA 2-1 NA UGIRIKI,YATUPWA NJE,COLOMBIA NA UGIRIKI ZAFUZU KUNDI C

 Cote d'Ivoire's golden generation taught tournament lesson by wily Greeks



IVORY Coast imekuwa timu ya pili ya Afrika kuaga mapema Kombe la Dunia nchini Brazil baada ya kufungwa mabao 2-1 na Ugiriki usiku huukatika mchezo wa mwisho wa Kundi C.
Mabao yaliyowazamisha Ivory Coast usiku huu yamefungwa na Giorgios Samaras dakika ya 42 na Samaras  90 na ushei kwa penalti.

 Wilfried Bony aliifungia bao pekee Ivory Coast dakika ya 74 katika mchezo ambao timu hiyo ilihitaji sare kwenda 16 Bora. Colombia imemaliza na ushindi wa 4-1 dhidi ya Japan na kufikisha pointi tisa, mbele ya Ugiriki yenye pointi nne, Ivory Cpast poiniti tatu na Japan pointi moja.
Kikosi cha Ugiriki kilikuwa; Ugiriki, Karnezis/Glykos dk26, Maniatis, Manolas, Samaras, Kone/Samaris dk11, Karagounis/Gekas dk24, Salpingidis, Torosidis, Lazaros, Sokratis na Cholevas.
Ivory Coast; Barry, Boka, Kolo Toure, Bamba, Serey 6; Kalou 6, Tiote/Bony dk61, Gervinho/Sio, dk83, Drogba/Diomande dk78, Aurier na Yaya Toure.

No comments:

Post a Comment