Kocha wa timu ya Uingereza Roy Hodgson atakitaja
kikosi cha taifa kitakachoshiriki katika kombe la dunia litakaloandaliwa
mwezi juni Brazil.
Timu hiyo vilevile imepangiwa kushiriki mechi zaidi za kirafiki dhidi ya kabla ya Honduras na Ecuador mjini Miami Marekani.
Uingereza iliyojumuishwa katika kundi D itafungua kampeni yake katika dimba la kombe la dunia tarehe 14 Juni dhidi ya Italia kisha ielekee Sao Paulo tarehe 19 Juni kumenyana na Uraguay kisha imalize udhia dhidi ya Costa Rica tarehe 24 Juni.
Mchezaji wa Uingereza anayechezea klabu ya Tottenham, Andros Townsend hatashiriki katika kombe la dunia baada ya kupata jereha katika kifundo cha mguu wake hapo jana.
No comments:
Post a Comment