tuwasiliane

Friday, April 25, 2014

KOCHA MPYA TAIFA STARS KUWASILI KESHO

 KOCHA
Kocha Mkuu mpya wa Taifa Stars, Martinus Ignatius Maria maarufu kama Mart Nooij anatarajiwa kuwasili nchini Kesho siku Jumamosi alfajiri (Aprili 26 mwaka huu) tayari kwa ajili ya kuanza kazi ya kuinoa timu hiyo.

Nooij (59) atawasili saa 7.20 usiku kwa ndege ya Ethiopia Airlines ambapo anatarajia kukutana na waandishi wa habari Jumamosi mchana, saa chache kabla ya kuanza mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars na Burundi itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mart Nooij ni raia wa Uholanzi, na ameshawahi kufanya kazi katika nchi ya Mozambique kama kocha mkuu wa timu ya taifa, Burkina Faso U20, na pia ameifundisha timu ya Santos ya Afrika ya Kusini.

No comments:

Post a Comment