picha ya kikosi cha zaman cha staz
Na Boniface Wambura, Addis Ababa I
TIMU
ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, jioni hii imetoka sare ya
bila kufungana na Sudan kwenye Uwanja wa Addis Ababa mjini hapa katika
mchezo wa kirafiki ulio kwenye kalenda ya Shirikisho la Soka la
Kimataifa (FIFA).
Taifa
Stars ambayo iko Addis Ababa tangu Jumatatu (Mei 27 mwaka huu) imeweka
kambi katika hoteli ya Hilton kujiandaa na mchezo wa Kundi C dhidi ya
Morocco Juni 8 mjini Marakech kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe
la Dunia mwakani nchini Brazil.
Stars,
inayodhaminiwa na kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya
Kilimanjaro Premium Lager, katika mchezo wa leo, iliwakosa wachezaji
wake wawili nyota, Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta ambao walikuwa
wanaichezea klabu yao, TP Mazembe ya DRC katika Kombe la Shirikisho
Afrika.
Washambualiji
wa Stars akina Khamis Mcha ‘Vialli’, Mrisho Ngasa na Amri Kiemba
wakiongozwa na John Bocco walilitia msukosuko mara kwa mara lango la
Sudan ambalo lilikuwa chini ya beki wa kati Nadir Eltayeb ambaye
alifanya kazi ya ziada dakika ya 72 kuokoa mpira uliokuwa ukielekea
wavuni.
Stars
katika mechi hiyo iliwakilishwa na Juma Kaseja, Nadir Haroub/Vincent
Barnabas, Shomari Kapombe, Kelvin Yondani, Aggrey Morris, Frank Domayo,
Mrisho Ngasa, Salum Abubakar, John Bocco/Haroun Chanongo, Amri
Kiemba/Khamis Mcha na Simon Msuva/Athuman Iddi ‘Chuji’. Baada ya mechi
hiyo, wachezaji wa Stars wamealikwa chakula cha usiku na Balozi wa
Tanzania nchini Ethiopia, Joram Biswaro, ambapo watakutana pia na baadhi
ya Watanzania wanaoishi Ethiopia kabla ya kuondoka kesho alfajiri
kwenda Morocco kwa kupitia Cairo, Misri ambapo inatarajia kuwasili
Casablanca saa 8 mchana.
Kocha
Kim Poulsen amesema kikosi chake kinaendelea na mazoezi vizuri na
kitaimarika zaidi baada ya Samatta na Ulimwengu kujiunga na wenzao kesho
huu mjini Marrakech.
No comments:
Post a Comment