tuwasiliane

Friday, June 14, 2013

Fastjet kutoa huduma za bei nafuu

 

Shirika la ndege, linalotoa huduma za usafiri wa ndege kwa bei nafuu Fastjet, limepata kibali cha kuanzisha safari za ndege za kimataifa za bei nafuu, kutoka Tanzania hadi Afrika Kusini, Zambia na Rwanda.
Kampuni hiyo inayomilikiwa na Stelios Haji-Ioannou, ambaye ni mmiliki wa shirika la ndege la Easyjet, lililo na makao yake barani ulaya.

Shirika hilo limetangaza kuwa litaanzisha safari za ndege katika mataifa hayo kwa bei nafuu huku abiria wakilipa dola mia moja pekee.
Kwa sasa shirika hilo linahudumia wasafiri nchini Tanzania pekee.

Raia wengi na hasa wafanya biashara wamefurahishwa na tangazo hilo, wakisema kuwa itapunguza gharama za usafiri na hivyo kuimarisha biashara katika kanda hiyo.

Nchini Kenya, shirika la ndege la Kenya Airways ambalo ni moja ya mashirika makubwa ya ndege barani Afrika, limepata pigo kubwa baada ya kupata hasara kubwa katika kipindi cha miaka minne iliyopita.
Ripoti zinasema kuwa shirika hilo lilipata hasara ya zaidi ya dola milioni mia moja kabla ya kutozwa ushuru, kiwango ambacho ndicho mbaya zaidi tangu mwaka wa 2009.
Shirika hilo lilikuwa maarufu sana kwa abiria wanaosafiri magharibi, mashariki, kusini na katika mataifa ya Afrika ya kati.

No comments:

Post a Comment