tuwasiliane

Tuesday, March 26, 2013

EXCLUSIVE: SERIKALI KUUNDA KAMATI YA USHINDI YA STARS - YASEMA ITAENDELEA KUMLIPA KIM POULSEN

Siku moja baada ya kuiongoza timu ya Taifa ya Tanzania kuitandika Morocco 3-1 na kujiweka kwenye nafasi nzuri kwenye michuano ya kugombania nafasi ya kushiriki michuano ya kombe la dunia 2014. Leo serikali kupitia naibu waziri wa michezo na habari Mh.Amos Makalla imesema itaendelea kumlipa mshahara kocha wa timu ya taifa Kim Poulsen.

Kim Poulsen ambaye alichukua nafasi ya Jan Poulsen mwaka jana kuiongoza timu ya soka ya wakubwa ya Tanzania, amekuwa na rekodi nzuri katika kuiongoza timu ya taifa kwenye kipindi kifupi alichokaa huku timu ikionyesha mwelekeo mzuri kwa kufanya vizuri kwenye michuano mbalimbali inayoshiriki.

Akizungumza na mtandao huu asubuhi ya leo Mh.Amos Makalla alisema: "Naipongeza sana Taifa Stars kwa ushindi walioupata, nawapongeza wachezaji kwa kujituma muda wote hakika wameijengea heshima Tanzania nawataka waongeze bidii wasibweteke! Nampongeza kocha mkuu na benchi la ufundi kwa muda mdogo ameijenga timu vizuri na amewaelewa wachezaji vizuri. Nawashukuru watanzania kwa kujitokeza kwa wingi na kuishangilia timu yao muda wote, aidha serikali inakusudia kuunda kamati ya kusaidia Taifa Stars ili kuongeza nguvu haraka iwezekanavyo ili kuiwezesha kufanya vema katika mechi zilizobaki! Pamoja na kamati serikali itaendelea kulipa mishahara wa kocha wa timu ya taifa." - alimaliza Makalla

No comments:

Post a Comment