tuwasiliane

Sunday, June 10, 2012

10 JUN.Prof George Saitoti afariki kwenye ajali ya ndege


Habari kutoka Kenya zinasema kuwa Waziri wa Usalama wa Ndani ,Profesa George Saitoti, na naibu wake, Orwa Ojode, wamefariki dunia katika ajali ya helikopta ya polisi katika eneo la Kibiku karibu na mji wa Ngong, takriban kilometa ishirini kutoka mji wa Ngong.

Abiria wote saba waliokuwa kwenye ndege hiyo wanaarifiwa kuteketezwa kwa kiasi wasichoweza kutambulika.

Kamishna wa polisi Mathew Iteere anaarifiwa kulekea katika eneo la ajali hiyo.

Walioshuhudia tukio hilo wanasema ndege ilishika moto ilipogusa ardhi kwenye eneo la Ngong Hills.

Bwana Saitoti aliwahi kuwa makamo wa rais na waziri wa fedha katika serikali ya Rais Moi, na akitarajiwa kugombea urais katika uchaguzi ujao.

No comments:

Post a Comment