
TIMU ya soka ya Coastal Union ya Tanga imewaacha wachezaji wake tisa wakiwemo Ally Ahmed ‘Shiboli’, Benard Mwalala na Ramadhan Wasso.
Pia timu hiyo ipo mbioni kumsajili kiungo wa zamani wa Simba ya Dar es Salaam, Mkenya Jerry Santo kwa nia ya kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.
Akizungumza na gazeti hili, Katibu Mkuu wa Coastal Union, Kassim El Siag alisema jana kuwa wachezaji hao tisa wapo huru kujiunga na timu nyingine yoyote na kuwataja kuwa ni Mwalala, Samueli Temi, Shiboli, Wasso, Enock John, Laurent Mugia, Bakari Mohamed, Daudi Changula na Francis Busungu.
Katibu huyo alisema moja ya sababu za kuchukua uamuzi huo ni kutokana na kushuka kwa viwango vyao vya uchezaji na kwamba wana matumaini makubwa timu yao mwakani itakuwa moto wa kuotea mbali.
Alisema Kamati ya Usajili ya Coastal Union inaendelea na harakati za kufanya usajili wa nguvu kuhakikisha wanafanya vizuri zaidi msimu ujao.
Wakati huohuo, Coastal ipo mbioni kumsajili kiungo Mkenya Jerry Santo, ambapo kwa mujibu wa Ofisa Habari wa klabu hiyo, Edo Kumwembe mazungumzo yanaendelea kuhusiana na kiungo huyo.
“Tuko kwenye usajili sasa hivi, tayari tumeishawanasa wachezaji wawili na sasa tuko katika hatu ya mwisho na Jerry Sant,” alisema Edo.
Aliwataja wachezaji ambao wamewasajili kuwa ni Nsa Job kutoka Villa Squad na kiungo Sudy Mohmed wa Toto Africans ya Mwanza.
No comments:
Post a Comment