tuwasiliane

Tuesday, May 22, 2012

22 MAY.Matibabu ya Sajuki kitendawili


Jumapili iliyopita msanii huyo aliondoka hapa nchini kuelekea Hospitali ya Saifee iliyopo nchini India kwa matibabu, ameshindwa kufanyiwa upasuaji mapema nchini huko alikokwenda kwa dhumuni la kupata matibabu.

Kwani hali ya msanii huyo imezidi kutengemaa kila kukicha, watanzania wote kwa ujumla wameombwa kuzidi kumuombea Msanii huyo aweze kurudi haraka katika hali yake ya kawaida.

Si mwingine bali ni yule Msaniiw a Filamu za hapa nyumbani na pia ni mtayarishaji mashuhuri wa filamu hizo Salum Juma Kilowoko ‘Sajuki’, ameshindwa kufanyiwa upasuaji mapema nchini India alikokwenda kwa matibabu.

Msanii huyo anasumbuliwa na tatizo la uvimbe pembeni ya ini, ambapo wataalamu wa afya wanadai kuwa ni dalili za ugonjwa wa Hepatoma (kansa ya ini).

Hapo wawali Sajuki alianza kwa kupata uvimbe sehemu tofauti katika mkono wake mmoja, lakini baadaye tatizo hilo lilihamia ndani na kuanza kupata maumivu makali pembeni ya ini.

Kwani Msanii huyo alikaririwa akisema kwamba madaktari walibaini ana uvimbe pembeni ya ini, tatizo ambalo limekuwa likinisumbua kwa muda mrefu.

Kutokana na hali hiyo, wadau mbalimbali wa Filamu wakiwemo wasanii waliweza kumchangia nyota huyo kiasi cha fedha ambacho alitakiwa kukipata ili kuweza kufanyiwa matibabu nje ya Tanzania.

Timu nzima ya HAPA NDIO KILA KITU inazidi kumuombea msanii huyo afanyiwe mapema upasuaji huo ili arudi katika hali yake ya kawaida na kuendelea na kazi zake alizokuwa akizifanya hapo awali.

1 comment:

  1. Mungu awe nae katika matibabu yake. Naamini atarudi ktk afya njema na kuendelea na kazi zake za kuielimisha na kuiburudisha jamii kupitia tasinia ya filamu.

    ReplyDelete