tuwasiliane

Saturday, March 31, 2012

31 MARCH.SIMBA , YANGA ZANG`AA


Magoli mawili kwa upande wa simba ambayo yalifungwa na Salum Machaku na Haruna moshi boban kwenye mchezo dhidi ya African Lyon,yameweza kuizidisha kung`aa kileni mwa liki kuu ya Vodacom

katika mchezo huo magoli yote ya simba yalipatikana katika kipindi cha kwanza.katika kipindi hicho simba walionekana kutawala vilivyo huku vijana wa Afrikan lyon walikuwa wakicheza mchezo wa kujihami zaidi

katika kipindi cha pili kila timu ilionekana kutaka kubadilisha hali ya mchezo kwa simba kuongeza magoli na Lyon kusawazisha lakini mchezo ulionekana kubalance na hadi mwisho matokeo yakabaki 2kwa simba na 0 kwa Afrikan lyon

KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI TANGA


goli lililofungwa na Hamisi kiiza kwa kichwa katika dakika ya 42 ya mchezo iliiwezesha yanga kuibuka na ushindi wa Goli 1-0 dhidi timu ya Coast union

kwa matokeo ya mechi za leo simbaimeendelea kuaa kileleni mwa ligi hiyo kwa kuwa na points 50 ikifuatiwa na timu ya Yanga ambayo imefikisha points 46 huku azamu ikishuka kwa nafasi moja hadi nafasi ya 3 kwa kuwa ina points 44

ligi hiyo ya vodacom itaendelea tena kesho kwa mchezo kati ya AZAM dhidi ya timu ya jkt ruvu mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa azam chamazi

No comments:

Post a Comment