
Pini jipya la Prof Jay (Kamili Gado) alilomshirikisha Marco Chali litaanza kufanyiwa shooting mapema wiki ijayo chini ya Adam Juma wa Visual lab.
Jay anasema hata husika hata kidogo katika kudirect video hiyo wala kuandika script, na kazi hiyo amewaachia maswahiba wake wa karibu kufanya kazi hiyo ambapo itaandikwa na Frank Gonga, Flaviana Matata, Marcochali, Luca (Bongo 5) na wengine, katika kuonyesha utofauti wa video hiyo na zinginezo.
"Naomba sana watu wajitokeze sana siku hiyo, tuonyeshe jinsi gani tulivyo kamili gado, african girls walivyo kamili gado" amesema Jay.
No comments:
Post a Comment