tuwasiliane

Wednesday, December 21, 2011

21 DEC.K-LYN ATAMANI KURUDI KWENYE GAME


Former Miss Tanzania, ambaye pia ni mwanamuziki ktk anga hizi za Bongo, namzungumzia mwanadada Jackquline Ntuyabaliwe ‘K-LYNN’, amesema anatamani kurudi katika game lakini anashindwa kutokana na kubanwa na kazi nyingi anazojishughulisha nazo kwa sasa.

Kwa mujibu wa mwanadada huyo mrembo anaamini mashabiki wake wamemmiss na wanamuhitaji ili aweze kutoa tena burudani lakini anawaomba waendelee kumsubiri kidogo akiwa anajiandaa na ujio wake mpya atakaokuja nao.

K-Lynn anasema kuna uwezekano mkubwa mwakani akarudi kwenye game huku akiwa na staili mpya ambayo inaweza kumtoa zaidi, “ninaweza kurejea katika game kwani muziki bado upo katika damu,” alimalizia.

No comments:

Post a Comment