tuwasiliane

Saturday, October 20, 2012

ANGUKO LA UCHUMI UGIRIKI LASABABISHA KLABU KUDHAMINIWA NA DANGURO - WACHEZAJI WAAHIDIWA MADEMU WAKISHINDA MECHII


Kama ilivyo kwa vitu vingi vingine nchini Ugiriki, klabu za soka nazo zimekumbwa na tatizo la anguko la uchumi, lakini moja ya kampuni ya biashara ambayo yenyewe haijaathiriwa sana na na anguko la uchumi, imeamua kuchukua jukumu la kuisadia klabu moja ya soka ya nchi hiyo iliyopo mjini Larissa.
Kutoka AP:

Wachezaji wa klabu ya Voukefalas wamelazimika kuvaa jezi za pinki zenye logo za "Villa Erotica" na Soula's House of History, wakiwa ndio wadhamini wao wao wapya baada ya nchi hiyo kupigwa na tufani la anguko la uchumi hivyo kupelekea serikali kupunguza matumizi na kuiacha klabu hiyo ikiwa kwenye hali mbaya ya kifedha.
Timu nyingine pia zimekuwa kwenye hali tete ya kiuchumi, kuna klabu moja inadhaminiwa na kampuni inayojishughulisha na masuala ya mazishi huku nyingine ikidhaminiwa na maduka ya kuuza vitafunwa aina ya kebab.
Mmiliki wa kampuni ya Soula's House of History, Soula Alevridou, amelipa zaidi ya €1,000 kuweka jina lake kwenye jezi za pink za Voukefalas, lakini waandaji wa ligi wanajaribu kuizuia klabu hiyo kuvaa jezi hizo kwenye mechi kutokana wanahisi haitaleta picha nzuri kwa mashabiki wenye umri mdogo japokuwa biashara ya kuuza mwili ni halali nchini Ugiriki.
Kwa mujibu wa AP, Voukefalas inahitaji kiasi cha €10,000 kwa mwaka na mwanamama Alevridou, ambaye ni mmiliki wa kampuni inayosimamia danguro amesema ameamua kuidhamini timu hiyo kutokana na kuipenda klabu hiyo na sio kwamba anataka kuitangaza biashara yake ambayo kwa mujibu wake hahitaji matangazo.

Voukefalas mpaka sasa wamepoteza mechi nne mfululizo, lakini Ms.Alevridou amehaidi "muda maalum" kwa wachezaji katika danguro lake ikiwa watashinda.

No comments:

Post a Comment