tuwasiliane

Wednesday, January 25, 2012

25 JAN. KAULI MPYA YA BOB JUNIOUR KUHUSU DIAMOND!



Mwimbaji/Producer wa SHAROBARO RECORDS Bob Juniour, leo amezungumza ukweli wake kwamba japo walimaliza ugomvi uliokuwepo kati yake na msanii mwenzake DIAMOND PLATNUMS, hajawah kuongea hata kwenye simu na msanii huyo kwa kipindi kirefu, toka walipopatana.
Bob amesema alipatana na DIAMOND ili kumaliza skendo zilizokua zikiandikwa na magazeti ya udaku kuwahusu wao, ishu ambazo ambazo ziliichukiza familia yake na fans wake ndio maana akaamua kupatana ili kuzinyamazisha hizo skendo.
akiongea exclusive na millardayo.com BOB JUNIOUR amesema “kiukweli sasa hivi mimi na DIAMOND hatuongei, na nimeufuta mpango wa kufanya nae chochote kwenye muziki”
mwishoni mwa mwaka jana wakati Bob Juniour alipofanya interview na Millard Ayo siku chache baada ya kupatana na Diamond, alisema huenda december mwaka jana wangefanya kolabo na kuungana kwenye consert moja ambayo ingethibitisha zaidi kwamba wamepatana.

No comments:

Post a Comment