tuwasiliane

Tuesday, January 24, 2012

24 JAN. Essien kuingoza Ghana dhidi ya Botswana


GHANA wamepata somo sahihi katika mechi za ufunguzi za Kombe la Mataifa ya Afrika na kusisitiza kuwa hakuna timu mbovu kwenye mashindano hayo.Black Stars waanza kampeni yao leo jijini Franceville kwa kuivaa Botswana huku kocha wao Goran Stevanovic akidai wanataka kuionyesha dunia kwanini Ghana inapewa nafasi ya kuchukua ubingwa huo.

Wachezaji wa Ghana wana morali ya hali ya juu kwenye kambi yao huko Villa Ngoni, lakini kiungo Sulley Muntari amesema hakuna mechi rahisi."Kama ukiangalia nini kilichotokea siku ya ufunguzi utakubalia kwamba hakuna mechi rahisi," alisema Muntari akizungumzia ushindi wa Zambia dhidi ya Senegal. "Tunajiamini vya kutosha, lakini hatupaswa kudharau timu yoyote."

Upande wa pili Botswana watashuka dimbani bila ya kiungo wake tegemeo Joel Mogorosi aliyejiengua kutokana na majeruhi. Mogorosi alivunjika mkono wakati wa mazoezi ya Zebra nchini Cameroon wiki iliyopita na nafasi yake imechukuliwa na Abednego Powell.

Zebra hao tayari walishampoteza kiungo wao Dipsey Selolwane aliyefungiwa kucheza mechi hiyo ya ufunguzi.
Zambia ilichapa Senegal timu inayoaminiwa kutwaa taji hilo, huku Sudan wakiacha maswali mengi kwa Ivory Coast pamoja na kuwa walishinda bao 1-0.

Katika mechi nyingine ya Kundi D, nahodha wa Mali, Seydou Keita huenda akakosa mechi ya kwanza ya fainali za Mataifa ya Afrika dhidi ya Guinea kutokana na maumivu.

Kiungo huyo wa Barcelona, ambaye alishika nafasi ya pili katika tuzo za Mchezaji Bora wa Afrika, ana maumivu ya goti na enka na huenda akakosa mechi hiyo ya Kundi D itakayochezwa huko Franceville, Gabon leo Jumanne.
Kocha Alain Giresse alikuwa na nia ya kumpanga Cheick Tidiane Diabate, ambaye ni mshambuliaji wa Girondins Bordeaux lakini mchezaji huyo pia ana maumivu ya misuli.

Vile vile Mahamane Traore, ambaye ni kiungo kutoka Metz, hajapona maumivu yaliyomfanya akosekane katika mechi za maandalizi.Keita ndiyo kwanza amerudi katika kikosi cha Mali baada ya awali kuwa amejitoa kwa madai kwamba viongozi wa soka hawatendi haki. Kocha Giresse ndiye aliyemshawishi kurudi katika kikosi hicho.

No comments:

Post a Comment