
ALIYEKUWA mbunge wa viti maalum kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Regia Mtema, ameagwa rasmi leo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Kilombero mkoani Morogoro kwa mazishi.
Mbunge huyo kijana alifariki kwa ajali ya gari huko Ruvu mkoani Pwani ambapo watu wangine saba waliokuwa katika gari lake walijeruhiwa vibaya.
Makamu wa Rais, Mohamed Bilal, aliongoza maelfu ya Watanzania katika kumwaga mbunge huyo.
No comments:
Post a Comment